Polisi nchini Ujerumani imefanya msako katika majengo kadhaa kusini magharibi mwa nchi hiyo ili kuwakamata  watu wanaojihusisha na usafirishaji haramu wa binadamu .

Jeshi la Polisi nchini humo tayari limeshapokea hati nne za kuwakamata na msako huo utaendelea kufanyika  katika nyumba 24 katika miji ya Mannheim, Karlsruhe na Worms.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa  na polisi  imesema watu hao wanaosafirishwa wanatokea  Mashariki ya Kati na eneo la Caucasus ambapo wakiingia wanapatiwa kazi za kufanya bila vibali vya makazi.

Mpaka sasa kundi la watu saba wameshakamatwa na wanaendelea kuchunguzwa  huku polisi  ikiendelea kuwafuatilia  wengine  wanaotuhumiwa kuhusika na usafirishaji wa watu na kuajiri wahamiaji bila vibali vya makazi.

Please follow and like us:
Pin Share