Shirika la Posta la Marekani limesema limeacha kupokea mizigo kutoka China bara na Hong Kong kwa muda usiojulikana.
Huduma ya barua haitaathiriwa na usitishaji huo, ilisema shirika hilo, ambalo lilikataa kutoa sababu ya uamuzi huo.
Hata hivyo, mnamo Jumanne sheria mpya zilianza kutekelezwa ambazo ziliziba mwanya ulioruhusu vifurushi vidogo vya thamani ya $800 (£ 641) au chini yake kutumwa Marekani bila kulipa ushuru au ada.
Ilikuwa moja ya hatua zilizotangazwa na Rais wa Marekani Donald Trump ambaye alitoa agizo la ulipaji ushuru wa ziada wa 10% kwa bidhaa zote zilizoingizwa Marekani kutoka China.