Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akishiriki Mkutano wa Kawaida wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika kwenye ukumbi wa Nelson Mandela uliopo Makao Makuu ya Umoja huo, Addis Ababa nchini Ethiopia tarehe 15 Februari, 2025.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mfalme wa Eswatini, Mswati III kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Kawaida wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU), Jijini Addis Ababa nchini Ethiopia tarehe 15 Februari, 2025.