Rais wa Rwanda Paul Kagame yuko mbioni kuongeza utawala wake wa miaka 24 kwa miaka mingine mitano katika ushindi wa kishindo, huku kura nyingi zikihesabiwa kutoka katika uchaguzi wa Jumatatu.

Ana 99.15% ya kura kufikia sasa, na takribani asilimia 79 ya kura zimehesabiwa, matokeo ya awali yaliyotangazwa na tume ya uchaguzi yanaonesha.

Mzee huyo mwenye umri wa miaka 66 tena hakukabiliwa na upinzani wowote mkubwa, huku viongozi hao wakipigwa marufuku.

Wapinzani wake wawili waligawana chini ya 1% ya kura.

Bw Kagame aliwashukuru Wanyarwanda kwa imani yao katika hotuba katika makao makuu ya chama chake cha Rwandan Patriotic Front (RPF).

“Hizi si takwimu tu, hata ikiwa ni 100%, hizi sio nambari tu. Wao wanaonesha kuamini, na hilo ndilo lililo muhimu zaidi,” Bw Kagame alisema.

Wapinzani wake, mwanamazingira Frank Habineza na mwandishi wa habari na mwandishi Philippe Mpayimana, wana 0.53% na 0.32% mtawalia.

Matokeo kamili yanatarajiwa kufikia tarehe 20 Julai na ya mwisho ifikapo tarehe 27 Julai.

Please follow and like us:
Pin Share