Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikagua moja ya sehemu ya kuchuja maji ya mradi wa Same-Mwanga-Korogwe mara baada ya hafla ya uzinduzi iliyofanyika Mwanga mkoani Kilimanjaro tarehe 09 Machi, 2025.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiteta jambo na Waziri Mkuu Mstaafu Mzee Cleopa David Msuya mara baada ya kufungua mradi wa Maji wa Same-Mwanga-Korogwe kwenye hafla iliyofanyika Mwanga mkoani Kilimanjaro tarehe 09 Machi, 2025. Mzee Msuya pia aliwahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Mwanga.
Taswira ya eneo la mtambo wa kutibu maji (Water treatment Plant ) katika mradi wa Maji wa Same-Mwanga-Korogwe uliopo wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro.