
Rais Dkt. Samia pamoja na viongozi hao wamejadili kuhusu utoaji wa huduma kwa watoto wenye mahitaji maalum hususan wenye changamoto ya afya ya akili. Viongozi hao wa Kanisa wameipongeza na kuishukuru Serikali kwa ushirikiano inaotoa kwa Kanisa hilo.
Aidha, kuhusu utoaji wa huduma kwa watoto wenye mahitaji maalum hususan wenye changamoto ya akili, Serikali imeahidi kushirikiana na Kanisa ili kujenga Kituo kikubwa zaidi ili watoto wengi waweze kupata huduma hiyo.


