JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Mzimu uliowanyoa mawaziri unahitaji tambiko Tanzania (3)

Wakati mawaziri walipobinywa kujiuzulu sikushangaa nilipomsikia mmoja wao, aking’aka mbele ya waandishi wa habari. Waziri huyo wa zamani alisema: “Nijiuzulu ili iwaje? Mimi siwezi kujiuzulu…” Pamoja na kujitetea kote na kurusha lawama kwa wasaidizi wake lakini panga la Rais halikumhurumia.

Mwenyekiti aparaganisha halmashauri Karagwe

*Adaiwa kuchota 270,000, yeye ajibu hoja zote

 

Halmashauri Wilaya ya Karagwe imeingia katika mgogoro mpya, baada ya madiwani na watendaji wengine kuanzisha harakati za kumg’oa Mwenyekiti wa Halmashauri, Kashunju Singsbert Runyogote, ambaye naye amejibu mapigo kwa kuzima harakati hizo.

La Waislamu Matinyi kapotosha

Katika Gazeti la JAMHURI la Jumanne Juni 12, 2012, kuna makala iliyoandikwa na Mobhare Matinyi akishutumu Waislamu kuhusiana  na madai yao mbalimbali, wanayoyalalamikia kila siku hapa Tanzania.

Gerezani na vitu feki Uingereza

MIAKA ya 1990 baada ya kubahatika kununua kagari kangu mgongo wa chura, nilipitia machungu baada ya kuibiwa saiti mira. Nilijaribu kujiganga bila mafanikio, kwa sababu nilikuwa nimejikung’uta kila senti mfukoni nami niwe na gari na kuliweka barabarani kwa kujidai.

Katiba Mpya, Tanzania Mpya

Mpendwa msomaji wa makala ya Katiba Mpya, Tanzania Mpya, wiki iliyopita nilianza kuzungumzia historia ya Muungano wetu, jinsi ulivyoanza kama fikra na utashi wa viongozi waasisi wa taifa letu la Tanzania.

 

Wakati haya yanatokea sikuwapo, lakini nafurahi kwa sababu nimeisoma vizuri historia ya nchi yangu. Historia inatueleza mambo mengi, na ni vyema hata kuujua mfumo wa Muungano tulionao ulitoka wapi na matatizo yalianzia wapi? 

Leo niendelee tulipoishia wiki iliyopita ili baadaye tupate kujibu swali la je, tunayo ya kujadili kuhusu Muungano? Kama tunayo, tuyajadili katika mtindo gani?

Wabunge waibane Serikali bila woga

Wabunge jana walianza kujadili Bajeti ya Serikali ya mwaka 2012/2013. Kama ilivyotarajiwa, mjadala wa bajeti ya mwaka huu wa fedha ni mkali.

 

Wiki iliyopita wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliitwa katika Kamati yao ambayo Mwenyekiti wake ni Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

 

Kufanyika kwa kikao hicho kulikuwa ni maandaizi ya kuwaweka sawa wabunge wa CCM ambao ndiyo wengi, waweze kuipitisha bajeti hiyo. Hilo ni jambo la kawaida katika mabunge, hasa yenye mseto wa wabunge wanaotokana na vyama vingi vya siasa.