JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Wabunge waibane Serikali bila woga

Wabunge jana walianza kujadili Bajeti ya Serikali ya mwaka 2012/2013. Kama ilivyotarajiwa, mjadala wa bajeti ya mwaka huu wa fedha ni mkali.

 

Wiki iliyopita wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliitwa katika Kamati yao ambayo Mwenyekiti wake ni Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

 

Kufanyika kwa kikao hicho kulikuwa ni maandaizi ya kuwaweka sawa wabunge wa CCM ambao ndiyo wengi, waweze kuipitisha bajeti hiyo. Hilo ni jambo la kawaida katika mabunge, hasa yenye mseto wa wabunge wanaotokana na vyama vingi vya siasa.

Yah: Saba Saba na vinyozi na wapigadebe tunakwenda wapi?

Wanangu, nawashukuruni kwa kusoma mambo ya zamani pamoja na kwamba yanawakera, kwa sababu wengi wenu mnaona kama historia na ambayo labda mengine hayakuwahi kuwaingia vichwani kwamba yaliwezekana na yalitekelezeka.

 

Niliwahi kuwaandikia barua hii kuwakumbusha juu ya barua ambazo tulikuwa tukiandika, na ilichukua mwezi au zaidi kumfikia aliyeandikiwa. Barua hiyo ilikuwa na ujumbe mzito haiyumkiniki zilikuwa habari za uzazi, ndoa, vifo, majanga na hata tukio la furaha kijijini kwetu.

 

Baada ya miaka kadhaa ya Uhuru tulianzisha Shirika la Posta na Simu ambalo wakati huo simu zote zilikuwa zikiunganishwa Dodoma kwenda katika mikoa mingine. Hii ilikuwa njia ya haraka sana ya mawasiliano, lakini haikuwa kwa watu wote, bali wachache tu waliochukulia jambo lao ni la haraka sana.

Bajeti ya kodi za bia, soda haitufikishi popote

WIKI iliyopita Waziri wa Fedha, Dk. William Mgimwa alitangaza bajeti ya mwaka 2012/2013. Nafahamu kuwa mpendwa msomaji umeishasoma mengi kuhusiana na bajeti hii. Kwa mantiki hiyo mimi sitajielekeza katika kuchambua nini kimeongezwa kodi au kupunguzizwa kodi kama ulivyo utamaduni wa makala nyingi.

Tunafahamu sote sasa kuwa bajeti hii ya shilingi trilioni 15 na ushehi hivi, imekuwa ya ujumla mno. Bajeti hii sikuiona kama inalenga kutatua tatizo la njaa, umeme, barabara mbovu, reli, viwanja vya ndege, elimu, afya au hata mahusiano ya jamii. Kiwango kilichotengwa nadiriki kukiita umwagiliaji wa matone (drip irrigation).

Hata Waziri Mgimwa aliyeisoma bajeti hii kwa mara ya kwanza maishani mwake, naamini hadi leo yupo kwenye mshangao. Hajasikia mshindo. Hakuna jipya lililotokana na tangazo lake la bajeti. Labda hizo Sh milioni 50 anazotarajia kupata kutokana na matajiri wenye kuweka majina yao kwenye magari binafsi. Kwa bahati mbaya ingetokea mimi ndiye Waziri wa Fedha, nchi hii ningeishitua mbavu.

Wabunge waibane Serikali bila woga

Wabunge jana walianza kujadili Bajeti ya Serikali ya mwaka 2012/2013. Kama ilivyotarajiwa, mjadala wa bajeti ya mwaka huu wa fedha ni mkali.Wiki iliyopita wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliitwa katika Kamati yao ambayo Mwenyekiti wake ni Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Juhudi za Lowassa kuihangaikia elimu zinapaswa kuungwa mkono

 

Naweza kumpenda au kumchukia sana Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa, lakini hata iweje sitajizuia kumuunga mkono mtu yeyote akifanya jambo jema au lenye tija kwa taifa.

 

Siku chache zilizopita, Lowassa aliongoza harambee iliyokusanya Sh. milioni 530 kutoka kwa wadau wa maendeleo ya elimu – fedha ambazo Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho yeye mwenyewe ni mwanachama wake, kilichangia Sh. milioni 20.

 

Ikulu kukarabatiwa kwa Sh bilioni 6

Wabunge kadhaa wamejiandaa kuhoji matumizi ya Sh bilioni 6 zilizotengwa kwa ajili ya ukarabati wa Ikulu. Kiasi hicho cha fedha kimetengwa katika bajeti ya mwaka wa fedha wa 2012/2013. Wabunge wanahoji kiasi hicho kikubwa hasa kutokana na kuonekana kuwa kila…