Latest Posts
Salaam za Maige kwa ‘waliomfitini’
*Aahidi kuendeleza mapambano bungeni
Hivi karibuni Mbunge wa Msalala, Ezekiel Maige, alirejea jimboni na kupokewa na wapigakura wake na kisha akawaeleza kilichomfanya ang’olewe kwenye nafasi ya Waziri wa Maliasili na Utalii. Ifuatayo ni hotuba yake kwa wapigakura.
Maradona, toka Mwanasoka Bora wa Dunia hadi teja la mihadarati
ALIZALIWA Oktoba 30, 1960 katika jiji la Buenos Aires, Argentina, kutokana na ndoa ya Diego Maradona na mkewe, Dalma Salvadore ambapo pia naye akaitwa Diego Maradona, kisha akatokea kuwa mwanasoka aliyetamba duniani.
Mzimu uliowanyoa mawaziri unahitaji tambiko Tanzania (3)
Wakati mawaziri walipobinywa kujiuzulu sikushangaa nilipomsikia mmoja wao, aking’aka mbele ya waandishi wa habari. Waziri huyo wa zamani alisema: “Nijiuzulu ili iwaje? Mimi siwezi kujiuzulu…” Pamoja na kujitetea kote na kurusha lawama kwa wasaidizi wake lakini panga la Rais halikumhurumia.
Mwenyekiti aparaganisha halmashauri Karagwe
*Adaiwa kuchota 270,000, yeye ajibu hoja zote
Halmashauri Wilaya ya Karagwe imeingia katika mgogoro mpya, baada ya madiwani na watendaji wengine kuanzisha harakati za kumg’oa Mwenyekiti wa Halmashauri, Kashunju Singsbert Runyogote, ambaye naye amejibu mapigo kwa kuzima harakati hizo.
La Waislamu Matinyi kapotosha
Katika Gazeti la JAMHURI la Jumanne Juni 12, 2012, kuna makala iliyoandikwa na Mobhare Matinyi akishutumu Waislamu kuhusiana na madai yao mbalimbali, wanayoyalalamikia kila siku hapa Tanzania.
Gerezani na vitu feki Uingereza
MIAKA ya 1990 baada ya kubahatika kununua kagari kangu mgongo wa chura, nilipitia machungu baada ya kuibiwa saiti mira. Nilijaribu kujiganga bila mafanikio, kwa sababu nilikuwa nimejikung’uta kila senti mfukoni nami niwe na gari na kuliweka barabarani kwa kujidai.