Latest Posts
Pangua pangua kubwa Tanesco
Uongozi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), umefanya mabadiliko makubwa kwa kuwaondoa katika vituo vya kazi, baadhi ya watumishi waliofanya kazi kituo kimoja kwa miaka mingi, JAMHURI imetibitishiwa. Katika mabadiliko hayo yaliyotarajiwa kutangazwa wakati wowote kuanzia jana, wafanyakazi 191 wamekumbwa na “hamisha hamisha” hiyo katika Mkoa wa Dar es Salaam. Kazi hiyo itafanywa kwa mikoa yote nchini.
Wabunge waichachafya Katiba
*Jaji Warioba, Mbunge walumbana ukumbini
Wabunge kadhaa wameikosoa Katiba ya sasa ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na wametoa mapendekezo mazito wakipendekeza yaingizwe kwenye Katiba mpya.
Kenya, Uganda, Rwanda wanatuacha solemba
Kwa zaidi ya wiki sasa nipo hapa Nairobi, Kenya, nikihudhuria mafunzo ya uandishi wa habari za masuala ya kifedha, hasa bajeti ya Serikali. Mafunzo haya ni ya muda wa wiki mbili. Katika mafunzo haya tunapewa mifano kutoka sehemu mbalimbali na wakubwa kutoka Serikali ya Kenya wanawasilisha mada.
Dk. Nagu alichomfanyia Sumaye
Barua hii imeandikwa na watu waliojitambulisha kuwa ni wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambao ni Wajumbe wa Mkutano Mkuu Wilaya ya Hanang’. Iliandikwa Oktoba 19, mwaka huu na kupelekwa kwa Katibu Mkuu wa CCM-Taifa. Kimsingi inapinga ushindi wa nafasi ya NEC wa Dk. Mary Nagu dhidi ya Waziri Mkuu mstaafu Frederick Sumaye.
YAH: KUPINGA MATOKEO YA UCHAGUZI NAFASI YA MJUMBE WA HALMASHAURI KUU TAIFA (NEC) WILAYA YA HANANG’
Mheshimiwa Katibu Mkuu, kichwa cha habari hapo juu chahusika. Sisi wenye majina na saini zetu hapo chini kwenye kiambatanisho cha barua hii ni viongozi na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM (W) ya Hanang’.
Mtikisiko mkubwa CCM
*Msekwa, Karume kutemwa rasmi, vigogo wengi kuangukia pua
*Wasira, Lukuvi, Membe, Makamba, Mukama wapambana
*Balozi Seif, Shamsi, Khatib, Mbarawa, Samia, Mwinyi vita kali
Wiki hii Chama Cha Mapinduzi (CCM) kitakuwa katika hatua za mwisho za kukamilisha safu zake za uongozi, huku mtikisiko mkubwa ukitarajiwa kutokea kwa vigogo wengi kubwagwa kwenye nafasi ya ujumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) – viti 10 Bara na viti 10 Zanzibar.
Maximo alishindwa, nani atamvumilia Boban?
Moja ya uamuzi mgumu uliofanywa na uongozi wa Klabu ya Simba ya Dar es Salaam, ni kumsimamisha mchezaji wake, Haruna Moshi ‘Boban’, kwa kosa la utovu wa nidhamu.