JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Misaada mingine ya Marekani ni fedheha

Wiki iliyopita Rais Jakaya Kikwete alizungumza neno zuri. Sina hakika kama viongozi wetu waliweza kulisikia na kulitafakari, kutoka kwenye hotuba ya kiongozi huyo wakati akizindua Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela, mkoani Arusha.

Simba wanataka Kaseja adake, awafungie mabao?

Wakati mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara ulimalizika Jumapili iliyopita, kipa namba moja wa klabu ya Simba na timu ya taifa (Taifa Stars), Juma Kaseja, amehitimisha ngwe hiyo kwa huzuni, mashaka na wasiwasi mkubwa kutokana na kutukanwa, lawama na vurugu alizofanyiwa kuanzia Morogoro hadi jijini Dar es Salaam.

Inawezekana kuzalisha fedha bila kutumia fedha

Watu wengi wamekuwa wakisema na kujiaminisha kauli kama hizi: “Tumia fedha kupata fedha,” “Siwezi kuanza biashara wakati sina fedha,” “Bila chochote ni vigumu kupata kitu,” “Wenye fedha ndiyo wanaofanikiwa,” na nyingine nyingi zinazofanana na hizo.

Nyerere: Paka na panya

“Inawezekana tatizo la paka kwa panya lingekwisha kama paka angefungiwa kengele shingoni; tatizo ni kumpata panya wa kuifanya kazi hiyo… Panya watakuwa wajinga sana wakidhani kuwa paka watajifunga au watafungana kengele shingoni.”

Haya ni maneno ya Baba wa Taifa letu, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, wakati akifafanua jinsi ilivyo vigumu kwa panya kuepuka kukamatwa na paka.

Ligi Kuu Bara ‘yaanza upya’

Ushindi wa Dar es Salaam Young Africans (Yanga) wa mabao 3-0 dhidi ya JKT Mgambo katika mashindano ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Jumatano iliyopita, na sare ya bao 1-1 kati ya mabingwa watetezi, Wekundu wa Msimbazi Simba Sports Club ya jiji na Polisi Morogoro siku hiyo, ulizifanya Yanga na Simba kufikisha pointi 23 kila mmoja. Hali ya kulingana pointi ya mahasimu hao wakuu wa soka nchini imeibua msisimko mpya kwa mashabiki wa pande zote.

EWURA waomba subira ya wananchi

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imekiri kutokuwapo kwa mafuta ya kutosha nchini, kutokana mvurugano wa meli zinazoingiza mafuta nchini.

Kauli hiyo imetolewa na Meneja Mawasiliano wa (EWURA), Titus Kaguo, alipozungumza na waandishi wa habari na kuwataka wanachi kuwa na subira wakati Mamlaka husika ikitafuta ufumbuzi wa kudumu wa suala hilo.