JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Mkono: Hata JK yapo ya Chadema anayoyakubali

*Aeleza sababu za kusaini kumng’oa Waziri Mkuu
*Asukumwa na wizi uliofanywa mgodini Buhemba

Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono (CCM), ameamua kueleza sababu zilizomfanya asaini fomu ya majina ya wabunge katika kusudio la kumpigia kura Waziri Mkuu Mizengo Pinda ya kutokuwa na imani naye.

Katiba mpya itakimudu kizazi cha ‘FACEBOOK?’

Suala la maisha na siasa ni kama lile fumbo la yai na kuku. Kipi kinaanza kati ya siasa na maisha. Ni siasa ndiyo inayozaa maisha ama ni maisha ndiyo yanayozaa siasa? Kipi ni mzazi wa kingine?

Waziri makini hawezi kusherehekea uteuzi

Rais Jakaya Kikwete amefanya mabadiliko makubwa katika Baraza la Mawaziri. Baadhi ya mawaziri na naibu mawaziri wamepoteza nafasi walizokuwa wakishikilia, kutokana na kashfa ya ufujaji wa fedha na mali nyingine za umma.

Waandamanaji kupinga unyonyaji wa Barrick

Mkutano wa mwaka huu wa Barrick Gold Mine uliofanyika Toronto, Canada, umeingia dosari ya maandamano.

Mkulo alivyopiga dili

[caption id="attachment_46" align="alignleft" width="314"]Mbunge wa Singida Mjini, Mohamed Dewji akiteta na Mbunge wa Iramba Mashariki, Mwigulu Mchemba[/caption]*Siri nzito zavuja alivyoishinikiza CHC iwauzie kiwanja Mohammed Enterprises
*Katika kumlinda Katibu Mkuu akanusha maelekezo aliyotoa Mkulo hotelini
*Soma mgongano wa kauli na nakala za mashinikizo ya Wizara ya Fedha kwa CHC

Siri nzito na zenye kuitia aibu Serikali juu ya mgogoro wa uuzaji wa kiwanja Na. 10 kilichopo Nyerere Road kwa kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (METL) zimeanza kuvuja.

Uchunguzi uliofanywa na Gazeti la Jamhuri kwa wiki tatu sasa na kufanikiwa kupata nyaraka nzito kutoka ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG), zinafanana kwa kila hali na nakala ya nyaraka zilizopo Wizara ya Fedha, unashitua.

KATIBA MPYA ITAKIMUDU KIZAZI CHA ‘FACEBOOK?’

“Nasema Katiba ya kweli ya Watanzania inapaswa kuandikwa katika mioyo na utashi wao, na wala si ya kuandikwa kama hii tunayoililia sasa”.