JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Messi wa Barcelona, Argentina ni kama Boko wa Azam na Tanzania

LICHA YA KUJITENGENEZEA REKODI NA KUTESA DUNIANI:

WIKI tatu zilizopita, mshambuliaji anayeaminika kuwa ndiye bora zaidi duniani hivi sasa, Lionel Messi, alivunja rekodi ya kuifungia mabao mengi zaidi timu yake ya Barcelona ya Hispania tangu ilipoundwa.

Waraka wa wanafunzi elimu ya juu nchini (1)

Ufuatao ni waraka wa wanafunzi wa elimu ya juu nchini kwa Serikali, kuhusu migomo na maandamano ya mara kwa mara hapa nchini. Umeandikwa na jopo la viongozi wa wanafunzi wa vyuo vikuu na wameupeleka serikalini. Wanatoa ushauri maridhawa wa namna ya kukomesha migomo kwa kuboresha sekta ya elimu, hasa kwa kuwapa fursa wanafunzi wote bila ubaguzi. Waraka huu ni mrefu na JAMHURI itauchapisha wote kuanzia leo. Endelea…

Wanaomiliki nyara za Serikali kukiona

Katika kukabiliana na wimbi la ujangili, Wizara ya Maliasili na Utalii imewataka watu wote wanaomiliki nyara za Serikali bila vibali, kujitokeza kueleza namna walivyozipata.

Operesheni za al-Shabaab zadhoofishwa Kenya

Operesheni za usalama zinazofanywa kwa msaada na jamii zimedhoofisha uwezo wa kundi la wanamgambo la al-Shabaab kufanya mashumbulizi nchini Kenya. Tangu Februari 17, wakati wanachama wa al-Shabaab waliposhambulia kituo cha polisi katika eneo la Jarajila mjini Garissa, na kumuua polisi mmoja, hapajatokea mashambulizi yoyote yanayohusishwa moja kwa moja na al-Shabaab katika eneo hili, Kamishna wa Jimbo la Kaskazini Mashariki, James ole Seriani, alisema mwishoni mwa wiki.

Kifo cha CCM ki wazi, suala ni lini kitatokea

Mengi yameandikwa juu ya ushindi wa Joshua Nassari wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika Jimbo la Arumeru Mashariki. Naomba wasomaji waniruhusu nami niweze kusema japo kwa ufupi mtazamo wangu juu ya ushindi wa kijana huyo.

Rais Jakaya Kikwete aahidi Katiba mpya 2014

Rais Jakaya Kikwete amesema Watanzania watakuwa na Katiba mpya ifikapo mwaka 2014. Alipoulizwa kama hilo litawezekana hasa ikizingatiwa kuwa Kenya iliwachukua miaka saba kuwa na Katiba mpya, alijibu kwa mkato, “Hao ni Kenya, sisi ni Tanzania.”