JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Wakubwa wanavyotafuna nchi

[caption id="attachment_27" align="alignleft" width="314"]Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Ludovick Utoah, akiwasilisha ripoti ya ukaguzi kwa mwaka wa fedha wa 2009/2010 kwa waandishi wa habari bungeni mjini Dodoma, wiki iliyopita[/caption]*Kampuni ya Mohamed Enterprises yauziwa viwanja kinyemela
*Bandari watumbua zaidi ya bilioni 1.5, waendesha miradi hewa
*Mabosi wanachomeka watumishi hewa, wanavuta mishahara

Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh, ya mwaka wa fedha unaoishia Juni 30, 2011; imeendelea kufichua namna kundi la watumishi wa umma na wafanyabiashara wakubwa wanavyoitafuna Tanzania. Utouh aliwasilisha taarifa hiyo bungeni mwishoni mwa wiki.

Ni vita ya rushwa, haki

Uchaguzi wabunge EALA…

Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano leo wanatarajia kuchangua wabunge tisa watakaoiwakilisha Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki (EALA).

CCM hofu tupu

[caption id="attachment_24" align="alignleft" width="267"]Rais Jakaya KikweteRais Jakaya Kikwete[/caption]Mwenyekiti Mkoa atoboa siri nzito
Wakati kukiwa na dalili za kuwapo uchaguzi mdogo Jimbo la Arusha Mjini, hali ya mambo ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) imeelezwa kuwa mbaya.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha, Onesmo ole Nangole, ameonyesha wasiwasi wake juu ya kukosekana kwa mshikamano na umoja ndani ya chama hicho kikongwe.

Mabiti azingatie onyo la wananchi wa Simiyu

Machi 28, mwaka huu wananchi wa Simiyu walimtahadharisha Mkuu wa Mkoa huo, Paschal Mabiti, dhidi ya genge la wafanyabiashara wakubwa wa pamba, vinginevyo “watamuweka mfukoni”. Mabiti aliyeteuliwa hivi karibuni kushika nafasi hiyo na kupangiwa kwenda huko, alikuwa Mkuu wa Wilaya…

Huyu ndiye Kanumba niliyemfahamu

Kulikuwa na vilio na simanzi Mtaa wa Vatican, Sinza Dar es Salaam, nyumbani kwa aliyekuwa mwigizaji maarufu ndani na nje ya Tanzania, Steven Charles Kanumba ‘The Great’. Kanumba alifariki dunia alfajiri ya kuamkia Aprili 7, mwaka huu.

Kimbembe cha petroli London kama Dar

Wakati Jiji la Dar es Salaam lilipokumbwa na zahama ya ukosefu wa mafuta na vurugu kwenye vituo vya petroli na dizeli, sote tulibaki vinywa wazi.