JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Wabongo roho mbaya hadi Ulaya?

Kuna watu huwa wanafikiria wenzao walio ughaibuni – Ulaya, Marekani au hata Mashariki ya Kati – ni wachawi. Halafu kuna wengine walikuwa wakisema kuwa labda waliotoka Tanzania na sehemu nyingine za Afrika kwenda huko na kupata maendeleo, walibebwa au ni kubarikiwa tu.

Kashfa mpya Maliasili

[caption id="attachment_73" align="alignleft" width="314"]KagashekiWaziri wa Maliasili na Utalii, Khamis Kagasheki[/caption]*Kiini macho chaibuka vitalu vya WMA
*Vyatangazwa Kagasheki akiapa Ikulu
*Ni kukamilisha ratiba, matajiri wavinasa

Waziri wa Maliasili na Utalii, Khamis Kagasheki, anakabiliwa na mtihani wa kwanza ndani ya wizara hiyo, baada ya kuibuka kwa kashfa mpya katika ugawaji vitalu 13 vya uwindaji vinavyomilikiwa na Jumuiya za Hifadhi za Wanyamapori (WMAs).

Vitalu hivyo ni tofauti na vile vilivyosababisha kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri wa wizara hiyo, Ezekiel Maige. Habari za uhakika kutoka ndani ya Wizara ya Maliasili na Utalii na katika WMA, zinaonyesha kuwa kutangazwa kwa vitalu hivyo kumefanywa haraka haraka siku Kagasheni na mawaziri wenzake walipokuwa Ikulu wakiapishwa.

Jaji Warioba natarajia urejeshe Tanganyika yetu (5)

Taifa letu Tanzania lipo katika mchakato wa kuandika Katiba mpya. Mchakato huu umekwishafikia hatua nzuri. Tayari Tume imepata wajumbe 32 wakiongozwa na Jaji Joseph Warioba. Tume hii imesheheni watu muhimu na jamii inaiamini kweli. Mimi ni mmoja wa watu wanaoiamini. Jaji Warioba naamini anaifahamu vyema Katiba yetu na pia Katiba za mataifa mengine.

TANESCO yapata mafanikio nchini

*Yafikishia umeme Watanzania asilimia 18.4, mita 65,000 za Luku zaingia
SHIRIKA la Umeme nchini (TANESCO) limeanza kupiga hatua kutokana na juhudi linazofanya za kuwafikishia umeme Watanzania walio wengi.

TCRA yakamilisha anwani za makazi

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imekamilisha mpango wa kuwapatia Watanzania anwani za makazi.

Teknohama inavyopaisha biashara

Katika zama hizi za utandawazi, dunia yetu imetawaliwa na mifumo ya aina nyingi inayotikisa na kugusa maisha kila siku ya wakazi wa dunia nzima. Moja ya mifumo hiyo ni mfumo wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEKNOHAMA) pamoja na mfumo wa biashara.