JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

La Waislamu Matinyi kapotosha

Katika Gazeti la JAMHURI la Jumanne Juni 12, 2012, kuna makala iliyoandikwa na Mobhare Matinyi akishutumu Waislamu kuhusiana  na madai yao mbalimbali, wanayoyalalamikia kila siku hapa Tanzania.

Gerezani na vitu feki Uingereza

MIAKA ya 1990 baada ya kubahatika kununua kagari kangu mgongo wa chura, nilipitia machungu baada ya kuibiwa saiti mira. Nilijaribu kujiganga bila mafanikio, kwa sababu nilikuwa nimejikung’uta kila senti mfukoni nami niwe na gari na kuliweka barabarani kwa kujidai.

Katiba Mpya, Tanzania Mpya

Mpendwa msomaji wa makala ya Katiba Mpya, Tanzania Mpya, wiki iliyopita nilianza kuzungumzia historia ya Muungano wetu, jinsi ulivyoanza kama fikra na utashi wa viongozi waasisi wa taifa letu la Tanzania.

 

Wakati haya yanatokea sikuwapo, lakini nafurahi kwa sababu nimeisoma vizuri historia ya nchi yangu. Historia inatueleza mambo mengi, na ni vyema hata kuujua mfumo wa Muungano tulionao ulitoka wapi na matatizo yalianzia wapi? 

Leo niendelee tulipoishia wiki iliyopita ili baadaye tupate kujibu swali la je, tunayo ya kujadili kuhusu Muungano? Kama tunayo, tuyajadili katika mtindo gani?

Wabunge waibane Serikali bila woga

Wabunge jana walianza kujadili Bajeti ya Serikali ya mwaka 2012/2013. Kama ilivyotarajiwa, mjadala wa bajeti ya mwaka huu wa fedha ni mkali.

 

Wiki iliyopita wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliitwa katika Kamati yao ambayo Mwenyekiti wake ni Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

 

Kufanyika kwa kikao hicho kulikuwa ni maandaizi ya kuwaweka sawa wabunge wa CCM ambao ndiyo wengi, waweze kuipitisha bajeti hiyo. Hilo ni jambo la kawaida katika mabunge, hasa yenye mseto wa wabunge wanaotokana na vyama vingi vya siasa.

Yah: Saba Saba na vinyozi na wapigadebe tunakwenda wapi?

Wanangu, nawashukuruni kwa kusoma mambo ya zamani pamoja na kwamba yanawakera, kwa sababu wengi wenu mnaona kama historia na ambayo labda mengine hayakuwahi kuwaingia vichwani kwamba yaliwezekana na yalitekelezeka.

 

Niliwahi kuwaandikia barua hii kuwakumbusha juu ya barua ambazo tulikuwa tukiandika, na ilichukua mwezi au zaidi kumfikia aliyeandikiwa. Barua hiyo ilikuwa na ujumbe mzito haiyumkiniki zilikuwa habari za uzazi, ndoa, vifo, majanga na hata tukio la furaha kijijini kwetu.

 

Baada ya miaka kadhaa ya Uhuru tulianzisha Shirika la Posta na Simu ambalo wakati huo simu zote zilikuwa zikiunganishwa Dodoma kwenda katika mikoa mingine. Hii ilikuwa njia ya haraka sana ya mawasiliano, lakini haikuwa kwa watu wote, bali wachache tu waliochukulia jambo lao ni la haraka sana.

Bajeti ya kodi za bia, soda haitufikishi popote

WIKI iliyopita Waziri wa Fedha, Dk. William Mgimwa alitangaza bajeti ya mwaka 2012/2013. Nafahamu kuwa mpendwa msomaji umeishasoma mengi kuhusiana na bajeti hii. Kwa mantiki hiyo mimi sitajielekeza katika kuchambua nini kimeongezwa kodi au kupunguzizwa kodi kama ulivyo utamaduni wa makala nyingi.

Tunafahamu sote sasa kuwa bajeti hii ya shilingi trilioni 15 na ushehi hivi, imekuwa ya ujumla mno. Bajeti hii sikuiona kama inalenga kutatua tatizo la njaa, umeme, barabara mbovu, reli, viwanja vya ndege, elimu, afya au hata mahusiano ya jamii. Kiwango kilichotengwa nadiriki kukiita umwagiliaji wa matone (drip irrigation).

Hata Waziri Mgimwa aliyeisoma bajeti hii kwa mara ya kwanza maishani mwake, naamini hadi leo yupo kwenye mshangao. Hajasikia mshindo. Hakuna jipya lililotokana na tangazo lake la bajeti. Labda hizo Sh milioni 50 anazotarajia kupata kutokana na matajiri wenye kuweka majina yao kwenye magari binafsi. Kwa bahati mbaya ingetokea mimi ndiye Waziri wa Fedha, nchi hii ningeishitua mbavu.