JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Mabomu Mbagala siri zavuja

*Wakubwa walitumia (msiba huo) kutengeneza utajiri binafsi
*Ofisi ya Pinda yahaha kutafuta zaidi ya bilioni fidia mpya
*Waliopunjwa kucheka, hundi hewa milioni 260 zadoda

Miaka mitatu baada ya mabomu kulipuka katika Kambi ya Jeshi Mbagala nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam, siri nzito zimeanza kuvuja jinsi wakubwa walivyotumia msiba huo kujitengenezea utajiri binafsi.

TANESCO yachachamaa, yasweka jela wezi wa umeme

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limechachamaa na kuanzisha operesheni kabambe inayoambatana na kuwasweka lupango wateja wake wanaoiba umeme.

Jaji Warioba tunatarajia urejeshe Tanganyika yetu – 7

Wiki iliyopita nilichambua kwa kina kifungu cha 32 hadi 46A cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania juu ya madaraka ya Rais. Sitarejea niliyoyaandika lakini nashukuru kwa mrejesho mzuri wenye mshindo nilioupata. Wakati toleo hilo linatoka nilikuwa Lushoto mkoani Tanga, kwenye mafunzo yanayohusiana na masuala ya Katiba yaliyoandaliwa na Baraza la Habari Tanzania (MCT).

Drogba kamaliza enzi zake Ulaya kwa mafanikio, heshima kubwa

Wiki moja iliyopita, mshambuliaji wa kimataifa wa Ivory Coast, Didier Drogba, aliwaaga wachezaji wenzake wa Chelsea baada ya kuitumikia timu hiyo kwa miaka minane akitokea Marseille mwaka 2004.

Wahitimu wa Kibongo wachangamkiwa London

Uzuri wa ng’ombe wa maziwa ni pale akishazaa na kuanza kutoa maziwa kwa wingi. Karibu sawa na hivyo, uzuri wa mwanafunzi machoni pa waajiri ni pale anapohitimu vyema masomo yake na kuwa tayari kwa kazi.

Napata wasiwasi kuhusu upotoshaji huu

Nimesoma makala katika gazeti moja litolewalo kila siku, yenye kichwa cha habari, “NIDA imemdhalilisha Rais, majeshi iombe radhi”. Katika makala hayo, mwandishi amejitahidi kuueleza umma kile anachoamini ni ukweli, wa taarifa zilizotolewa katika vyombo vya habari nchini na baadaye kuja kufafanuliwa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), kuhusu sakata la vyeti 948 vya majeshi yetu kuwa feki (kughushi).