JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Brigedia Jenerali Aliasa Taifa

*Asema udini na ukabila ni ufa unaobomoa Taifa letu

 

Moja ya hotuba za Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, zisizochujuka ni ile aliyoitoa pale Kilimanjaro Hotel mbele ya Klabu ya Waandishi wa Habari Tanzania Machi 13, 1995.

 

Katika mazungumzo yake siku ile alitaja nyufa tano zinazolitikisa  Taifa letu kuanzia kwenye paa, katika dari, kutani hadi kufikia katika msingi ule imara wa Taifa uliojengwa kwa muda mrefu. Nyufa zilizotajwa zilikuwa:-

 

* Muungano

* Kupuuza na kutojali

* Kuendesha mambo bila kujali sheria

* Rushwa, na

* Ukabila na udini.

 

Mchechu NHC ameonyesha njia, wakurugenzi wengine mko wapi?

Wiki iliyopita Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limepata mkopo wa wastani wa Sh bilioni 165. Shirika limeupata mkopo huu kutoka benki na mashirika tisa ya fedha. Mashirika na benki zilizotoa mkopo huu na kiasi cha fedha walizotoa kwenye mabano ni CRDB Bank (Sh 35 bilioni), ECO Bank (Sh 20 bilioni), ABC (Sh 4 bilioni), NMB (Sh 26 bilioni), CBA (Sh 24 bilioni), TIB (Sh 22 bilioni), Azania (Sh 7 bilioni), Local Authorities Pension Fund-LAPF (Sh 15 bilioni) na Shelter Africa Company (Sh 22 bilioni).

 

Dk. Ulimboka siri zavuja

*Uchunguzi waanza kuleta majibu yenye utata
*Yadaiwa madaktari walimshitukia, wakamteka
*Madaktari wasisitiza serikali haiwezi kujinasua

Siri za uchunguzi wa awali wa tukio la kutekwa na kujeruhiwa kwa Dk. Stephen Ulimboka zimeanza kuvunja, lakini kwa mshangao wa wanaojua kilichotokea, uchunguzi huo unatoa majibu yenye tata.

Kamati ya Jumuiya ya Madaktari Tanzania yapinga Tume

Lifuatalo ni tamko la Jumuiya ya Madaktari Tanzania kwa waandishi wa habari walilolitoa Juni 28, mwaka huu juu ya Tume iliyoundwa na Polisi kuchunguza kutekwa na kupigwa kwa Dk. Stephen Ulimboka.

 

Madaktari wote hatuna imani na Tume iliyoundwa na Jeshi la Polisi nchini yenye lengo la kuendesha uchunguzi juu ya kutekwa, kunyanyaswa na kupigwa vibaya kwa Dk. Stephen Ulimboka na tunataka chombo huru kiundwe ili kupata ukweli wa tukio hilo.

 

Natabiri Nyalandu atakuwa tatizo

Siku chache baada ya uteuzi wa viongozi wakuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii – waziri na naibu wake, niliandika waraka mahsusi uliowahusu. Moja ya mambo niliyoyazungumza ni namna wizara hii ilivyo na vishawishi vingi vinavyotokana na ukwasi wake.

 

Hotuba ya jk

 

Kuna madai ya madaktari yasiyotekelezeka – Rais Kikwete

Mapema mwezi huu, Rais Jakaya Kikwete alihutubia Taifa kama ilivyo ada ya utaratibu wake aliojiwekea kila mwezi. Pamoja na mambo mengine, Rais Kikwete alizungumzia mgomo wa madaktari ulioathiri huduma za afya katika baadhi ya hospitali za umma nchini. Ifuatayo ni sehemu ya hotuba hiyo iliyogusia suala la mgomo wa madaktari.