JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Muhongo, Maswi wanatisha

 

*Gharama za kuunganisha umeme zakuna wengi

*Migodi yote si hiari tena kulipa kodi ya mapato

*Afuta mashangingi ya bure, vigogo watakopeshwa

*Mnyika, Selasini wawanyoosha wabunge wala rushwa

 

Wananchi wengi wameeleza kufurahishwa na msimamo wa uongozi mpya wa Wizara ya Nishati na Madini wa kuwapunguzia wananchi ukali wa gharama za kuunganisha umeme, kufuta ununuzi wa mashangingi na kuwabana wenye migodi mikubwa kuanza kulipa kodi ya mapato.

 

Haya ndiyo mambo murua yanayoliliwa na Watanzania

Wizara ya Nishati na Madini imetangaza kupunguza gharama za kuunganishia wateja wake umeme. Gharama hizo zimepungua kwa wastani wa asilimia 30 na 77. Uamuzi huo ulitangazwa na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, bungeni mwishoni mwa wiki.

Biashara za sasa zinahitaji u-sasa

Wakati baba yangu mzazi akifariki katikati ya miaka ya 1990, alikuwa mmoja wa wafanyabiashara waliokuwa wakipanda kwa kasi kubwa kibiashara. Akiwa ameshakusanya uzoefu wa kusafiri kibiashara hadi nchi jirani ikiwamo Malawi, alifariki dunia na kuacha biashara zilizokuwa zimestawi kweli kweli.

Danadana za Sheria ya Habari zitaisha lini?

Wiki iliyopita Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, Dk. Fenella Mukangara, amewasilisha bajeti ya wizara yake kwenye mkutano wa Bunge unaoendelea mjini Dodoma. Si nia yangu kujadili bajeti hii inayofikia wastani wa Sh bilioni 19. Na wala sitajadili danadana ilizopigwa bajeti hii, ambayo awali ilikuwa iwasilishwe Julai 18, lakini kwa mshangao ikasogezwa ghafla hadi Agosti 7, kisha kinyemela ikarejeshwa Julai 24.

Wabunge, Nishati acheni mivutano

 

Ijumaa wiki hii Wizara ya Nishati na Madini inatarajiwa kuwasilisha bajeti yake bungeni. Kama ilivyo kawaida tayari harakati zimeanza. Wabunge wanapigana vikumbo, Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco William Mhando amesimamishwa kazi na Wizara ya Nishati na Madini  inapambana na upatikanaji wa umeme.

Ewura yaokoa bilioni 170/-

*Ni baada ya kudhibiti uchakachuaji kwa kuweka vinasaba

*Wabunge waliotemeshwa ulaji wanaanza harakati ivunjwe

 

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imeliwezesha taifa kuokoa zaidi ya Sh bilioni 170 kwa mwaka, lakini hatua hiyo imewakera baadhi ya wabunge waliokuwa wakichakachua na sasa wanafanya mbinu ivunjwe.