JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Dk. Lwaitama: Serikali tatu hazikwepeki

 

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Azavel Lwaitama (pichani), amesema suluhisho pekee la kunusuru Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni kuwa na Serikali tatu.

Dk. Lwaitama alitoa kauli hiyo katika Mazungumzo ya Asubuhi kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yaliyoandaliwa na Baraza la Habari Tanzania na kufanyika katika Hoteli ya Court Yard jijini Dar es Salaam jana.

Serikali yaelekea kukubali hoja ya Waislamu

Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), inaelekea kulikubali ombi la kundi la waumini wa Kiislamu wanaotaka dodoso la dini liingizwe kwenye Sensa ya Watu na Makazi iliyopangwa kufanyika Agosti 26, mwaka huu.

Uamuzi huo ambao umeshawahi kupingwa na Mkurugenzi Mkuu wa NBS, Dk. Albina Chuwa, unatajwa kwamba huenda ukatangazwa hivi karibuni baada ya ngazi ya juu ya uongozi “kutafakari” na kubaini kuwa dodoso hilo haliwezi kuathiri umoja na mshikamano miongoni mwa Watanzania.

Biashara za sasa zinahitaji u-sasa

Ingawa kuna mambo mengi hapa katika u-kisasa, kwa leo nitagusia maeneo matatu tu. Mosi, kuweka biashara katika mifumo rasmi; pili kuwa na maono; na tatu kutengeneza mfumo wa kurithisha biashara kutoka baba kwenda kwa watoto – kutoka kwa wajukuu kwenda kizazi cha pili. Biashara katika mifumo rasmi ina dhana pana, lakini kwa urahisi kabisa ni kuendesha biashara katika mifumo inayoelezeka. Ni ile hali ambayo mmiliki unapokuwapo au kutokuwapo biashara inaendelea kama kawaida.

Niliyojifunza ufunguzi wa Olimpiki

JIJI hili sasa hivi hakuna kingine kinachozugumzwa wala kusikilizwa kupita michezo ya Olimpiki. Nimekubali kwamba ni michezo mikubwa na faida yake kwa waandaaaji si ndogo.

Ukishaona watu wanafanya kampeni kubwa kama Uingereza ili tu waandae kitu hiki kwa mara ya tatu, lazima ujue kuna manufaa.

HOTUBA YA WAZIRI WA NISHATI NA MADINI

HOTUBA YA WAZIRI WA NISHATI NA MADINI MHESHIMIWA PROF. SOSPETER MWIJARUBI MUHONGO (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA  MATUMIZI  KWA MWAKA 2012/13

Hotuba iliyowazima  wabunge mafisad

Bunge linanuka rushwa. Baadhi ya wabunge wanapokea rushwa ili kutetea maslahi ya wanaowatuma. Lakini wapo wabunge jasiri walioamua kupambana na wenzao wala rushwa kama inavyothibitishwa na Hotuba ya Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Wizara ya Nishati na Madini,…