JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Hongera Mkapa, Kikwete alijiandalia aibu ya Mahalu

Napata wakati mgumu. Napata shida jinsi ya kuanza makaha haya. Napata shida si kwa sababu nina maslahi binafsi, bali kwa sababu nakumbuka hadithi ya mwanafunzi aliyebeba upodo huku akijifunza kurusha mishale ya sumu. Hakuwa mahiri na hakujua jinsi ya kuvuta upinde. Kwa kicheko kikubwa, aliipaka sumu ncha ya mshale, upinde akauelekeza karibu na tumbo lake, kamba ya kurushia mshale ikatokea mbele yake.

Barua ya kibiashara kwa BRELA

Baada ya kuandika makala ya “Biashara za sasa zinahitaji u-sasa”, kuna jambo nililitazamia ambalo limetokea kama yalivyokuwa matarajio yangu. Kumekuwa na wasomaji wengi nchi nzima ambao wameleta maombi na ushauri wakitaka niwasaidie kusajili biashara zao katika mfumo wa kampuni.

Ni aibu TFF, ZFA kugombea Sh milioni 12 za mgawo wa BancABC

Wiki iliyopita, Shirikisho la Kandanda Tanzania (TFF) lililazimika kuutolea ufafanuzi mvutano wa mgawo wa fedha za michuano ya BancABC Super 8 kati yake na Chama cha Soka cha Zanzibar (ZFA), kilipotishia kuziondoa timu zake. Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah, aliwaambia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuwa fedha zote zilizotolewa na wadhamini wa michuano hiyo – BancABC – zimelipwa kila sehemu kunakohusika zikiwamo timu zote zinazoshiriki, viwanja vinavyotumika, miji inakochezwa na promosheni ya masoko iliyogharimu shilingi milioni nane.

Olimpiki: Kweli kupanga ni kuchagua

Leo nimeazima busara ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, aliyesema kwamba kupanga ni kuchagua.

Uongozi wa Mwalimu Nyerere haujapata kutokea, si Tanzania tu bali katika nchi nyingi za dunia, hata kama katika hili kuna wale wasioambilika. Kama mipango yote aliyokuwa ameisuka na kuanza kutekeleza Mwalimu ingepata wasimamiaji wazuri, nakuapia leo tungeweza hata kuandaa michezo ya Olimpiki.

Denis Vedasto: Mjasiriamali aliyekuta na JK

“Niliona  ni vyema nikuze kipaji changu kuliko kitumike na watu wengine kwa kuajiriwa, kwani nina ubunifu mkubwa kuliko ndiyo maana niliona ni bora nianzishe kampuni yangu.” Hayo ni maneno ya Denis Vedasto, mkazi wa Kitunda, Dar es Salaam ambaye ni mjasiriamali anayejishughulisha na utengenezaji wa vitanda vya hospitali, ambavyo vingine hutumiwa wakati wa kinamama kujifungua.

Dk. Lwaitama: Tuboreshe, tusivunje Muungano

Nimesikitishwa na aina ya uandishi wa habari  uliojiweka wazi  katika taarifa iliyonukuliwa kuandikwa na mwandishi wa gazeti moja la kila siku  (Tanzania Daima la Agosti 7, 2012), Datus Boniface.  Huyu mwandishi, pamoja na wahariri wake walioruhusu habari hiyo kuchapwa  walithubutu kusema uongo kuwa  eti “ Dk Lwaitama, Prof. Sheriff na Prof Shivji waliushambulia Muungano.” Tena, mwandishi huyu na wahariri walioruhusu habari hiyo ichapishwe  wakaenda mbali zaidi na kutumia  kichwa  cha habari kilichosema eti ‘Shivji, Lwaitama wataka Muungano uvunjwe’.