JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Kung’ang’ania sensa isusiwe ni upuuzi

Sensa ya idadi ya watu na makazi inafanyika kuanzia Jumapili wiki hii hadi Septemba 2, huku baadhi ya Watanzania wakiendelea kuipinga hadi dodoso la dini litakapojumuishwa. Viongozi mbalimbali wa Serikali hususan Wakuu wa Mikoa na Wilaya wamekuwa wakiwaomba viongozi wa kisiasa na kidini kuwataka waumini wao washiriki kikamilifu kuhesabiwa kwa sababu ni faida yao wenyewe na taifa letu.

Mkurugenzi: Ilala jitokezeni sensa

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ilala, Gabriel Fuime, amewataka wakazi wa Ilala kujitokeza kwa wingi kushiriki sensa ya watu na makazi inayofanyika kuanzia Jumapili wiki hii. Fuime aliiambia JAMHURI mwishoni mwa wiki kuwa kuna umuhimu mkubwa wa wakazi wa Ilala kujitokeza kwenye sense, kwani bila kufanya hivyo mgawo wa fedha kutoka serikalini utapungua.

Bunge lisiposema, wabunge watasema

 

Nimemsikiliza Naibu Spika Job Ndugai akilalamika kwamba nidhamu ya baadhi ya wabunge, hasa vijana si nzuri. Ndugai anarejea matukio kadhaa yaliyotokea wakati wa Mkutano wa Bunge ulioahirishwa wiki iliyopita. Alikwenda mbali zaidi kwa kukumbuka mambo yalivyo tangu kuanza kwa Bunge la Kumi. Analalamika kwamba asilimia zaidi ya 70 ya wabunge wa sasa ni wageni. Kuna vijana wengi ambao bado hawajazisoma na kuzitambua vema Kanuni za Kudumu za Bunge.

Ripoti ya majangili yatoka

*Wamo Polisi, Kada CCM, wafanyabiashara

*Vigogo Polisi Kigoma, Mugumu wahusishwa

 

Idara ya Ulinzi, Kitengo cha Intelejensia cha Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), imetoa ripoti ya ujangili iliyo na majina ya wahusika wakuu na namna wanavyolindwa na vyombo vya dola  nchini. JAMHURI imepata ripoti hiyo ya kurasa 30 iliyosainiwa na Mhifadhi wa Intelejensia, Renatus Kusamba.

Buriani Mbogora, bado sisi tunahangaika na Malawi

 

Moyoni nina majonzi. Natumia neno hili kwa vile siamini macho yangu, lakini ndivyo ilivyo. Hili linatokana na kifo cha mwanahabari mwandamizi, Alfred Mbogora. Nilimwona Mbogora siku moja kabla ya kifo chake, lakini zamu hii hakuwa akifahamu kama nilifika kumjulia hali katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, lakini angalau alitikisa mkono na mguu nilipoingia wodini. Hii ilikuwa Ijumaa.

Je, wote tuwe wajasiriamali?

Nianze kwa kushukuru na kutambua mirejesho ya wasomaji wa safu hii ambao wanaongezeka kila wiki. Mirejesho mnayoniletea kwa ujumbe mfupi wa maandishi, kupiga simu na kuniandikia baruapepe ina thamani na umuhimu mkubwa sana katika kunogesha safu hii.