JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Uhuru wa habari na magazeti kwa wote

Gazeti la JAMHURI ni miongoni mwa midomo, macho na masikio ya Watanzania na wadau wengine wa habari. Uhuru wa habari – ambao dunia yote inautangaza na kuuenzi kwa sasa – ni haki ya kila raia na chombo cha habari.

Bila kuheshimu Katiba tutayumba

Kwa wiki kadhaa sasa kumekuwapo mjadala mkali kuhusu uhalali wa baadhi ya majaji na sifa zao za kuifanya kazi hiyo. Kumekuwapo madai kwamba baadhi ya majaji wameteuliwa ilhali wakiwa na rekodi mbaya za uombaji rushwa, uonevu, upendeleo na kukosa uadilifu.

URAIS 2015

 

*Vikumbo vyaanza uchaguzi NEC-CCM

*Matayarisho ya mitandao yapamba moto

*Sura mpya, waliopotea waanza kuibuka

*Kipimo cha kukubalika ni kwenye NEC

Harakati za kuwania nafasi mbalimbali, hasa ujumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), zimetafsiriwa kwamba ni maandalizi ya kuelekea kwenye kinyang’anyiro cha urais mwaka 2015.

Siri zaanza kuvuja rushwa Kamati za Bunge

 

Mtandao wa wafanyabiashara wahusishwa

Kamati ya Maliasili, Mazingira yaguswa

Mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira aliyejitambulisha kuwa ni mpinga vitendo vya rushwa, ameamua kuandika makala hii kueleza baadhi ya vitendo vya rushwa ndani ya Kamati hiyo. Hii ni sehemu ya makala ya mbunge huyo ambaye kwa sasa tunalihifadhi jina lake.

UTANGULIZI

Tarehe 28 Julai 2012, Bunge la Tanzania liliingia katika historia baada ya Spika Anne Makinda kutangaza kuivunja Kamati ya Nishati na Madini pamoja na kamati nyingine zinazotuhumiwa kwa rushwa.

Spika alifikia hatua hiyo baada ya kuwapo kwa harakati za wafanyabiashara wa sekta ya mafuta kufanya mipango kwa zaidi ya wiki mbili za kuwashawishi wabunge washinikishe kujiuzulu kwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, na Katibu Mkuu Eliakim Maswi kwa kile kinachodaiwa kutoa zabuni kwa kampuni ya Puma Energy ya kuiuzia mafuta Tanesco kwa ajili ya mitambo ya umeme wa dharura ya  IPTL. Harakati zililenga wabunge wengi wenye ushawishi bungeni, wakianzia na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya

TFF yaanza kuiharibu Ligi Kuu

ALIPOCHAGULIWA kuwa Rais wa Kwanza wa Shirikisho la Kandanda Tanzania (TFF), beki wa zamani wa kimataifa wa Yanga na Pan African, Leodgar Chillah Tenga alitarajiwa kuleta mapinduzi makubwa ya soka hapa nchini.

Kikwete: Hakuna vita

“Namhakikisha ndugu yangu, watu wote wa Malawi kwamba hatuna nia wala mpango wa kuingia vitani. Hatuna matayarisho ya Jeshi wala jeshi halijasogea popote… mimi ndiye kamanda mkuu wa jeshi na sijapanga wala kutoa maelekezo ya vita.”   Haya ni maneno…