JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Wachezaji wa kigeni wanazididimiza Tanzania, England soka la kimataifa

 

Tangu ilipofuzu kushiriki fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zilizofanyika nchini Nigeria mwaka 1980, ikatolewa mapema ikiwa kundi moja na wenyeji, Misri na Ivory Coast, timu ya soka ya taifa ya Tanzania hadi sasa haijaweza kuifikia tena hatua hiyo na hakuna matumaini yoyote kama itafanya hivyo tena.

Msekwa ang’olewa Bodi Ngorongoro

*Orodha ya kwenda Ikulu jina lake lakatwa

*Ukomo wake ni Oktoba 5 mwaka huu

*Kilio cha kina Telele, Sendeka chasikika

Jina la Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Pius Msekwa, halimo katika orodha ya majina ya watu wanaopendekezwa kushika wadhifa huo, JAMHURI imethibitishiwa.

Njooni shambani mtajirike

Miezi kadhaa iliyopita kupitia Redio TBC Taifa, ofisa mmoja wa Wizara ya Maliasili na Utalii aliulizwa swali hili, “Je, inawezekana watu binafsi kufungua mashamba ya miti na kufanya biashara ya kuuza miti ya mbao?”

CWT: Mkombozi au mnyonya walimu?

*Nusu ya mapato yake yanatumika makao makuu

*Walimu wanaendelea kukamuliwa asilimia mbili

 

Mbunge wa Sumve, Richard Ndassa, katika Mkutano wa Bunge uliomalizika hivi karibuni alichangia Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na kuhoji matumizi ya mabilioni ya shilingi yanayofanywa Makao Makuu ya Chama cha Walimu Tanzania (CWT). Ifuatayo ni sehemu ya hotuba ya mbunge huyo.

Tumechagua kujenga taifa la wajinga

Kwa muda sasa nimekuwa nikifuatilia mwenendo wa elimu nchini. Nafuatilia kilio na matangazo yanayotolewa kila pahala, yakielezea wanafunzi zaidi ya 5,000 wanaomaliza elimu ya msingi na kufaulu mtihani wa darasa la saba huku hawajui kusoma na kuandika. Si hilo tu lakini nafuatilia pia kaulimbiu kuwa ‘Ualimu ni wito’.

Kila mmoja analalamika

 

Sifa mpya ya Watanzania sasa ni kulalamika. Malalamiko yameshamiri katika kaya, mitaa, ofisi, sehemu zote za kazi na kila mahali. Kinachosumbua zaidi ni kuona kuwa hakuna aliye tayari kuondoa malalamiko hayo hata kama mwenye dhima hiyo ni yeye mwenyewe.