JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Wabunge wengine wahongwa tena

 

* Mfanyabiashara tajiri wa Dar es Salaam ahusika

* Baadhi yao waogopa, wazisalimisha kwa Spika

Mfanyabiashara mwenye asili ya Kiasia amewahonga wabunge kadhaa wa Kamati ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala, JAMHURI imethibitishiwa. Habari za uhakika kutoka kwa baadhi ya wabunge na Ofisi ya Spika zinasema kwamba rushwa hiyo ilitolewa kama “asante” kwa wabunge hao baada ya kuzuru moja ya vitegauchumi vya mfanyabiashara huyo kilichopo Barabara ya Nyerere, Dar es Salaam, wiki kadhaa zilizopita.

Migogoro ya ardhi ni janga

Mhariri,

 

Kila siku migogoro ya ardhi inaripotiwa katika nchi yetu. Kuanzia Dar es Salaam hadi mikoani ni migogoro tu.

Mabaraza ya Kata yamesahaulika

Mhariri

 

Mabaraza ya Kata yameanzishwa kwa mujibu wa Sheria Na. 7/85 lakini halmashauri zinazosimamia mabaraza haya zimeyatelekeza kabisa. Mimi ni Katibu wa Baraza la Kata Kwashemshi. Tangu tuteuliwe mwaka jana hakuna mafunzo yoyote yaliofanyika, kitendo ambacho ni hatari sana. Mabaraza haya yamepunguza sana mlundikano wa kesi katika Mahakama za Mwanzo na Baraza la Ardhi na Nyumba Wilaya. Napenda niishauri Serikali yangu kwamba elimu kwa wajumbe hawa ni muhimu sana, kwani ni sehemu nyingi wajumbe wanalalamika kwamba wametelekezwa. Tatizo hili halipo kwa Baraza la Kata Kwashemshi tu bali mabaraza mengi nchini malalamiko ni haya haya.

Waziri Kagasheki atazame kasoro hii

Mhariri   Kwanza tunampongeza Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki kwa jitihada anazozifanya za kusafisha Wizara ya Maliasili na Utalii na Taasisi zake kwa jumla kwa kuondoa uozo uliokuwamo ndani kwa kipindi kirefu.   Wakati jitihanda hizo zikifanyika,…

Mandela: Urafiki na adui yako

“Ikiwa unataka kupata amani na adui yako, unapaswa kufanya kazi na adui yako, kisha anageuka na kuwa mdau wako.” Haya ni maneno ya Rais wa Kwanza wa Afrika Kusini, Nelson Mandela aliyemaliza vita ya ubaguzi wa rangi kwa kutumia mfumo…

Mgogoro wa Tanzania, Malawi ngoma mbichi

*Malawi waendelea kukomaa wachukue ziwa lote

*Tanzania yasema mgawo ni nusu kwa nusu tu

*Wazee wa hekima Afrika kuitwa kusuluhisha

*Wasipoafikiana kutinga Mahakama ya ICJ

*Yote hayo yakishindikana JWTZ wataamua

 

Kumekuwapo desturi ya wanasiasa kutafuta jambo la kuwawezesha kuwajenga kisiasa, ili waweze kushinda uchaguzi, hasa Uchaguzi Mkuu. Mzozo wa mpaka wa Ziwa Nyasa unaozihusisha nchi za Tanzania na Malawi unatajwa kuwamo mwenye mtiririko huo wa kidesturi. Malawi inatarajia kuingia kwenye Uchaguzi Mkuu mwaka 2014, hivyo kete inayotumiwa na chama cha Rais Joyce Banda, pamoja na vyama vingine vya siasa ni kutaka kutunisha msuli kupitia mzozo wa mpaka kati yao na Tanzania kwa lengo la kujipa kuungwa mkono na Wamalawi wengi.