JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Yah: Nguvu ya maji yaja, mtaua wangapi?

Wanangu, ka-jua ka leo kananikumbusha mandhari ya miaka mingi kabla Tanganyika haijaanza kuwa jangwa la kutisha na kushindwa kuhimili hali ya ukame na wakati mwingine kukosa maji ambayo yanasababisha hadi tukose umeme na kusababisha kuyumba kwa uchumi  wa mtu mmoja mmoja na nchi.

Kikwete polisi wanaanza kuyeyusha heshima uliyojijengea

Mwaka 2008 nilibahatika kuwa mmoja wa watu waliopata fursa ya kusafiri na Rais Jakaya Kikwete kwenda jijini Washington, Marekani. Safari hii ilikuwa ikihusiana na mambo mbalimbali lakini kubwa ni kushawishi Serikali ya Marekani kuridhia Mpango wa Millennia Challenge Cooperation (Account) – MCC.

Waziri Mgimwa ahimiza ufanisi PPF

Waziri wa Fedha, Dk. William Mgimwa, amehimiza utendani makini utakaongeza ufanisi katika Mfuko wa Pensheni za Mashirika ya Umma (PPF) nchini.

Elimu ya Tanzania vipi?

Baada ya matokeo ya mitihani ya darasa la VII ya mwaka 2011 kutangazwa, kumetokea tashtiti kubwa katika nchi hii. Kule kutangazwa kwamba wanafunzi 5,200 hawajui kusoma wala kuandika, lakini wamo miongoni mwa watoto 567,567 waliochaguliwa kuingia kidato cha kwanza mwaka huu, kumewashangaza wengi. Naona kama ni jambo fulani la kisanii!

Sumaye, Nagu katika vita kali

*Muhtasari wa kikao wachakachuliwa, jina la Dk. Nagu laingizwa

Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Wilaya ya Hanang’ mkoani  Manyara, kinakabiliwa na mpasuko unaosababishwa na uhasama ulioibuka kati ya Waziri wa Uwekezaji na Uwezeshaji, Dk. Mary Nagu, na Waziri Mkuu mstaafu Frederick Sumaye.

Kagasheki afyeka Kamati ya Vitalu

*Awatupa Jaji Ihema, Beno Malisa, Daniel Nsanzugwanko

*Pia wamo Mbunge Mwanjelwa, Kijazi, Profesa Rutashobya

*Chanzo ni tuhuma za rushwa ugawaji vitalu vya uwindaji

Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, ameifuta kazi Kamati ya Ushauri wa Ugawaji Vitalu vya Uwindaji wa Kitalii. Kamati hiyo, pamoja na mambo mengine, imelalamikiwa mno kwa vitendo vya rushwa miongoni mwa wajumbe wake zaidi ya 10.