JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Kuwafutia leseni hakutoshi, washitakiwe

Mojawapo ya habari zilizobeba uzito katika gazeti hili ni ile inayohusu uchakachuaji wa mbolea, ambao umekuwa ukichangia kudhoofisha juhudi za wakulima katika kujiondolea umaskini.

Rais Kikwete tuokoe Karagwe, Runyogote anatumaliza

Mheshimiwa Rais na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jakaya Mrisho Kikwete, Salaam. Mei 30, 2012, madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe, walimwandikia Mkurugenzi Mtendaji barua wakimtaka aitishe kikao maalumu cha Baraza la Madiwani, kujadili tuhuma mbalimbali za ufisadi walizozielekeza kwa Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Kashunju Runyogote.

Hatima ya taifa la wavivu, watunga sera mezani

Mwaka 1946  nilipangiwa na mkoloni kuwa Afisa Kata mashuhuri iliyojulikana kama Liwale, wakati huo ilikuwa na watu wapatao kama elfu mbili tu na kwa kweli walikuwa wengi kiasi cha kunifanya nigawe maeneo mengine yatawaliwe na vijana wenzangu niliowaamini.

Matajiri wahujumu kilimo nchini

Wakati Tanzania ikipambana kujiondoa katika adha ya njaa kwa kuboresha kilimo nchini kupitia mradi wa Kilimo Kwanza, wafanyabiashara wenye uchu wa utajiri wa haraka wanahujumu kilimo. Matajiri hawa wanapewa fedha za ruzuku kusambaza mbolea, lakini wanafanya kufuru. Kinachotokea, badala ya kuwapelekea wakulima mbolea, wanawapelekea mbolea iliyochanganywa saruji, chumvi na mchanga.

Fedha za rushwa Hanang’ zatisha

 

 

 

Vita ya kuwania nafasi ya NEC kupitia Wilaya ya Hanang’ Mkoa wa Manyara, imechukua sura mpya baada ya mmoja wa wagombea wanaoelezwa kuenguliwa kwenye Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Hanang’ kubuni mbinu mpya za kampeni.

 

Mzungu aiweka Serikali mfukoni

Raia anayesadikiwa wa Ubelgiji anayetafutwa na Serikali kwa ukwepaji kodi wa zaidi ya Sh bilioni 10, Marc Rene Roelandts, analindwa na baadhi ya watumishi na viongozi wa Serikali, JAMHURI imeelezwa. Kwa sasa mfanyabiashara huyo yuko mafichoni nje ya nchi kutokana na tuhuma zinazomkabili, lakini habari zinasema watumishi wake wawili wamekamatwa.