JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Tujihadhari unafiki usitunyime rais bora 2015

Uchaguzi Mkuu ujao hauko mbali kiasi cha kufanya Watanzania wachelewe kuanza maandalizi mapema. Ndiyo maana wengi hatushangai kuona na kusikia wanasiasa wanaojipanga sasa kwa ajili ya uchaguzi huo.

Utaifa hauna dini (2)

Licha ya kuwa na huo msimamo usiofungamana na dini yoyote, kati ya hizo mbili -uislamu wala ukristu- makundi yote mawili wakati ule waislamu wenye Koranic Schools ukanda wa mwambao hawakuzipokea shule hizi za Serikali.


Na wamisheni kwa wakati huo huo wakailaumu Serikali eti kwanini walianzisha shule hizi zenye mwegemeo wa kuwapendeza waislamu wale wa mwambao. Mawazo potofu kama haya yanaonekana katika maandishi mbalimbali ya wakati ule toka kila upande.

Uuzwaji ardhi Bagamoyo waitisha Serikali

 

* DC atoa tamko kali, awaonya wavamizi

* Ataka wanunuzi wafuate kanuni, sheria

* Ashauri wenyeji wabakize ya kuwasaidia

* Mifugo yailemea wilaya, aipiga marufuku


Serikali katika Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani, imewataka wananchi wawe makini katika uuzaji ardhi, kutokana na wimbi la Watanzania na raia wa kigeni wanaojitwalia ardhi kubwa wilayani humo.

 

Bomu la elimu litailipukia Tanzania

Mwishoni mwa wiki, gazeti la Serikali la Daily News limekariri kundi la wanafunzi wakitoa kilio kueleza masikitiko yao kuwa wameshindwa kupata mikopo kutoka Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB), na hivyo kuna wasiwasi kuwa hawataingia vyuoni mwaka huu. Kundi kubwa la wanafunzi waliohojiwa ni la watoto kutoka familia masikini.

Yah: Cheusi ndicho cha hela, kekundu na kekundu utaliwa

Wanangu, naanza kwa kusema nawapenda sana na siku zote nitakuwa pamoja nanyi katika maombi, ili mpate kuwa na siku nyingi za kuishi kama mimi nilivyobarikiwa  kutimiza miongo mingi kidogo. Nimefika miongo hiyo kutokana na kuwaheshimu wazazi wangu ambao ni miungu wangu hapa duniani.

Asante RC Mwambungu, Inspekta Anna

Septemba 28 ni siku ya pekee maishani mwangu. Ilikuwa ni siku mbili tu tangu niliposafiri na kufika Songea mkoani Ruvuma. Nilipanga katika hoteli iliyopo katikati ya mji iitwayo Safari Lodge.