JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Salaam za Maaskofu wa KKKT kwa Watanzania wote kuhusiana na matukio ya kuchoma moto makanisa ya Kikristo eneo la Mbagala, Dar es Salaam

WAPENDWA KATIKA BWANA, Waumini wa KKKT, Wakristo Wote na Watanzania kwa Ujumla. Neema na Iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba na Bwana wetu Yesu Kristo, Amina. Sisi maaskofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), tumepokea kwa…

Polisi wampuuza Kikwete

*Amri yake ya mwaka 2006 yaota mbawa

Jeshi la Polisi limepuuza agizo halali la Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais Jakaya Kikwete, lililolitaka lihakikishe linawasomesha watoto watatu wa askari polisi, PC Abdallah Marwa.

Upendeleo watoto wa wakubwa

 

*Watoto wengine wa vigogo wajazwa Idara ya Afya

*Washika nafasi zote za Jiji, Ilala, Temeke, K’ndoni

Siku chache baada ya kuibuka mjadala wa kuwapo watoto wengi wa vigogo ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), hali kama hiyo imejitokeza tena kwenye Idara ya Afya katika Jiji la Dar es Salaam na manispaa zake tatu za Temeke, Ilala na Kinondoni, JAMHURI imebaini.

Kibadeni ashirikishwe kukabili rushwa Ligi Kuu

Kocha Mkuu wa timu ya Kagera Sugar ya Bukoba, King Abdallah Kibadeni (Mputa), amekuwa wa kwanza kuzungumzia hadharani tuhuma za rushwa katika michezo ya Ligi Kuu ya Vodacom, Tanzania Bara.

Drogba kustaafu soka kifua mbele?

Nahodha na mshambuliaji mahiri wa timu ya taifa ya Ivory Coast (The Elephants), Didier Drogba, amefanikiwa kupata nafasi ya mwisho ya kucheza katika fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (CAN) 2013, zitakazofanyika nchini Afrika Kusini.

Nyerere: Kataeni kukandamizwa

“Watanzania watakuwa ni wajinga na mataahira, kama watakubali kuendelea kukandamizwa na watu wachache katika nchi yao wenyewe….”

Baba wa Taifa letu, Mwalimu Julius Nyerere, aliyasema hayo kuwahimiza Watanzania kupinga vitendo vya ukandamizaji ndani ya nchi yao.