JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Dk. Nagu alichomfanyia Sumaye

Barua hii imeandikwa na watu waliojitambulisha kuwa ni wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambao ni Wajumbe wa Mkutano Mkuu Wilaya ya Hanang’. Iliandikwa Oktoba 19, mwaka huu na kupelekwa kwa Katibu Mkuu wa CCM-Taifa. Kimsingi inapinga ushindi wa nafasi ya NEC wa Dk. Mary Nagu dhidi ya Waziri Mkuu mstaafu Frederick Sumaye.

YAH: KUPINGA MATOKEO YA UCHAGUZI NAFASI YA MJUMBE WA HALMASHAURI KUU TAIFA (NEC) WILAYA YA HANANG’

Mheshimiwa Katibu Mkuu, kichwa cha habari hapo juu chahusika. Sisi wenye majina na saini zetu hapo chini kwenye kiambatanisho cha barua hii ni viongozi na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM (W) ya Hanang’.

 

Mtikisiko mkubwa CCM

*Msekwa, Karume kutemwa rasmi, vigogo wengi kuangukia pua

*Wasira, Lukuvi, Membe, Makamba, Mukama wapambana

*Balozi Seif, Shamsi, Khatib, Mbarawa, Samia, Mwinyi vita kali

Wiki hii Chama Cha Mapinduzi (CCM) kitakuwa katika hatua za mwisho za kukamilisha safu zake za uongozi, huku mtikisiko mkubwa ukitarajiwa kutokea kwa vigogo wengi kubwagwa kwenye nafasi ya ujumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) – viti 10 Bara na viti 10 Zanzibar.

Maximo alishindwa, nani atamvumilia Boban?

Moja ya uamuzi mgumu uliofanywa na uongozi wa Klabu ya Simba ya Dar es Salaam, ni kumsimamisha mchezaji wake, Haruna Moshi ‘Boban’, kwa kosa la utovu wa nidhamu.

Watanzania tunapaswa kuongeza ‘akili ya fedha’

Mapema Julai mwaka huu, nilikutana na mzee mstaafu kutoka moja ya wilaya za mkoani Iringa. Mzee huyu ambaye ndiyo kwanza amestaafu  ualimu, nilimfahamu kwa njia ya simu kupitia kwa rafiki yangu. Haja ya mzee huyu ilikuwa tukutane nimsaidie kutafuta gari aina ya Hiace anunue.

Lini viongozi wakuu watakuwa wakuu?

Hatuhitaji ushahidi mwingine wa kutusaidia kutambua kuwa viongozi wetu ni kama wameshindwa kuliongoza Taifa letu. Rushwa na vurugu za kidini katika nchi yetu zilianza kama cheche za moto. Watawala (si viongozi) wakazipuuza. Wakaziacha, na sasa tunayaona matunda yake.

Trafiki wanakula kwenye daladala Dar es Salaam?

*Baadhi ya madereva, makondakta ni miungu watu

Usafiri wa daladala katika Jiji la Dar es Salaam siku hizi ni mithili ya mfupa unaoelekea kumshinda fisi. Baadhi ya madereva na makondakta ni miungu watu! Sijui wanakula pamoja na askari wa usalama barabarani (trafiki)?