JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Ushindi mgogoro Ziwa Nyasa ni wetu – Membe

*Wazee wataka waruhusiwe watumie ‘nguvu za miujiza’

“Inawezekana shetani kaingia. Huku Tanzania tuna uwezo hata wa kutumia ungo…mimi nimekulia hapa, mpaka ni katikati ya ziwa…Kama ninyi (Serikali) hamna bunduki, wananchi wapo tayari kupigana kwa kutumia fito…Hatutakufa mpaka tuone mwisho wa mgogoro huu, tupo tayari hata kwa kutumia miujiuza yetu,” Haya ni maneno ya  Mzee Anyosisye Mwakenja (80) wa Kijiji cha Matema Beach.

Hivi haya ya Tanzania ni ‘majiji’ au ni ‘mazizi’?

Wiki iliyopita Tanzania imeongeza jiji jingine kwenye orodha yake. Arusha imeungana na majiji mengine yaliyoitangulia- Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya na Tanga. Mamilioni ya shilingi yametumika kwenye uzinduzi rasmi uliofanywa na Rais Jakaya Kikwete, wakati wa ziara yake mkoani Arusha. Kitu cha maana zaidi kilichofanywa na Rais Kikwete kwenye ziara hiyo ni uzinduzi wa Chuo cha Nelson Mandela, kitakachosaidia kuibua na kuendeleza vipaji katika fani ya sayansi hapa nchini.

Waingereza wanapoanza kufukua makaburi

*Walionyanyaswa na Savile walikuwa wapi akiwa hai?

Mwaka uliopita nilikuwa miongoni mwa maelfu ya watu waliokuwa mitaa ya Roundhay, Leeds, baada ya kifo cha Jimmy Savile.

Pangua pangua kubwa Tanesco

Uongozi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), umefanya mabadiliko makubwa kwa kuwaondoa katika vituo vya kazi, baadhi ya watumishi waliofanya kazi kituo kimoja kwa miaka mingi, JAMHURI imetibitishiwa. Katika mabadiliko hayo yaliyotarajiwa kutangazwa wakati wowote kuanzia jana, wafanyakazi 191 wamekumbwa na “hamisha hamisha” hiyo katika Mkoa wa Dar es Salaam. Kazi hiyo itafanywa kwa mikoa yote nchini.

Wabunge waichachafya Katiba

*Jaji Warioba, Mbunge walumbana ukumbini

Wabunge kadhaa wameikosoa Katiba ya sasa ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na wametoa mapendekezo mazito wakipendekeza yaingizwe kwenye Katiba mpya.

Kenya, Uganda, Rwanda wanatuacha solemba

Kwa zaidi ya wiki sasa nipo hapa Nairobi, Kenya, nikihudhuria mafunzo ya uandishi wa habari za masuala ya kifedha, hasa bajeti ya Serikali. Mafunzo haya ni ya muda wa wiki mbili. Katika mafunzo haya tunapewa mifano kutoka sehemu mbalimbali na wakubwa kutoka Serikali ya Kenya wanawasilisha mada.