JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Ligi Kuu Bara ‘yaanza upya’

Ushindi wa Dar es Salaam Young Africans (Yanga) wa mabao 3-0 dhidi ya JKT Mgambo katika mashindano ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Jumatano iliyopita, na sare ya bao 1-1 kati ya mabingwa watetezi, Wekundu wa Msimbazi Simba Sports Club ya jiji na Polisi Morogoro siku hiyo, ulizifanya Yanga na Simba kufikisha pointi 23 kila mmoja. Hali ya kulingana pointi ya mahasimu hao wakuu wa soka nchini imeibua msisimko mpya kwa mashabiki wa pande zote.

EWURA waomba subira ya wananchi

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imekiri kutokuwapo kwa mafuta ya kutosha nchini, kutokana mvurugano wa meli zinazoingiza mafuta nchini.

Kauli hiyo imetolewa na Meneja Mawasiliano wa (EWURA), Titus Kaguo, alipozungumza na waandishi wa habari na kuwataka wanachi kuwa na subira wakati Mamlaka husika ikitafuta ufumbuzi wa kudumu wa suala hilo.

Mjasiriamali na nguvu ya fedha

Katika maisha yangu, ninaamini na kusimamia mambo makubwa matatu – ujenzi wa roho, ujenzi wa familia na ustawi wa kiuchumi. Naamini kuwa mafanikio ya kweli katika nyanja zote za maisha lazima yaanzie rohoni mwa mtu.

Ndugu zangu, nchi inateketezwa

Wapendwa, nimeshindwa kujua simanzi hii iliyonipata niielekeze kwa nani. Kilio hiki nakileta kwenu ili kwa pamoja tuweze kupata jibu la hiki kinachojaribu kukieleza hapa.Wiki iliyopita nilisafiri kutoka Dar es Salaam hadi Kyela mkoani Mbeya kwa kutumia gari. Nilirejea Dar es Salaam kwa usafiri huo huo. Njiani nilishuhudia mambo kadhaa ambayo naomba sana ndugu zangu tushirikiane kuyajadili.

Dalili ya kudidimia kwa uongozi bora Afrika

 

TUZO YA MO IBRAHIM KUKOSA MSHINDI

 

Nimesikitishwa na habari za Tuzo ya Mo Ibrahim kukosa mshindi mwaka huu, zilizotangazwa hivi karibuni na Kamati ya tuzo hiyo ambayo ni zawadi yenye thamani kubwa dunaini. Tuzo hiyo ilianzishwa mwaka 2006 na bilionea wa nchini Sudan, Mo Ibrahim, kwa ajili ya marais wastaafu wa nchi za barani Afrika.

 

JKT ni mtima wa Taifa (1)

Nimefurahishwa sana na tamko la Mkuu mpya wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Raphael Muhuga, alilolitoa Ikulu Septemba 26, mwaka huu, mara tu baada ya kuapishwa kwake kushika wadhifa huo.