JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Mukama chupuchupu

*Wasira, January Makamba, Lukuvi waongoza

*Mikakati ya kumwangushya Membe yakwama

Uchaguzi wa wajumbe 10 wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, umeshuhudia vigogo wakiibuka washindi huku Katibu Mkuu wa chama hicho, Wilson Mukama, akiponea tundu la sindano.

Mwekezaji auziwa Polisi

 

*Kituo kuhamishwa, polisi wanaoishi hapo kuondolewa

*Kunajengwa maduka, hoteli, hospitali, kumbi za starehe

*Wizara ya Mambo ya Ndani: Ardhi inaendelea kuwa yetu

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi imeingia mkataba na kampuni ya Mara Capital, kampuni tanzu ya Mara Group, unaoipa mamlaka kampuni hiyo kuchukua eneo lote la Polisi Oysterbay, Dar es Salaam, kwa ajili ya ujenzi wa duka kubwa la kisasa (shopping mall), hoteli mbili na huduma nyingine za kibiashara.

Misaada mingine ya Marekani ni fedheha

Wiki iliyopita Rais Jakaya Kikwete alizungumza neno zuri. Sina hakika kama viongozi wetu waliweza kulisikia na kulitafakari, kutoka kwenye hotuba ya kiongozi huyo wakati akizindua Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela, mkoani Arusha.

Simba wanataka Kaseja adake, awafungie mabao?

Wakati mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara ulimalizika Jumapili iliyopita, kipa namba moja wa klabu ya Simba na timu ya taifa (Taifa Stars), Juma Kaseja, amehitimisha ngwe hiyo kwa huzuni, mashaka na wasiwasi mkubwa kutokana na kutukanwa, lawama na vurugu alizofanyiwa kuanzia Morogoro hadi jijini Dar es Salaam.

Inawezekana kuzalisha fedha bila kutumia fedha

Watu wengi wamekuwa wakisema na kujiaminisha kauli kama hizi: “Tumia fedha kupata fedha,” “Siwezi kuanza biashara wakati sina fedha,” “Bila chochote ni vigumu kupata kitu,” “Wenye fedha ndiyo wanaofanikiwa,” na nyingine nyingi zinazofanana na hizo.

Nyerere: Paka na panya

“Inawezekana tatizo la paka kwa panya lingekwisha kama paka angefungiwa kengele shingoni; tatizo ni kumpata panya wa kuifanya kazi hiyo… Panya watakuwa wajinga sana wakidhani kuwa paka watajifunga au watafungana kengele shingoni.”

Haya ni maneno ya Baba wa Taifa letu, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, wakati akifafanua jinsi ilivyo vigumu kwa panya kuepuka kukamatwa na paka.