JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Wazungu Mererani wasalimu amri

Kampuni ya TanzaniteOne Ltd inayochimba madini ya tanzanite katika eneo la Mererani mkoani Manyara, hatimaye kuanzia wiki hii italazimika kuachia asilimia 50 ya hisa zake zimilikiwe na wazalendo, imethibitishwa.

Yaliyotikisa Mkutano wa Tisa wa Bunge

Mkutano wa tisa wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ulihitimishwa Novemba 9, mwaka huu, mjini Dodoma, ukiwa umetikiswa zaidi na hoja binafsi za wabunge; Kabwe Zitto, Halima Mdee na hukumu ya Spika wa Bunge, Anne Makinda.

Chadema vaa miwani muone CCM walipoangukia

Wiki iliyopita Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemaliza mkutano wake wa Nane. Katika mkutano huu kimemchagua Mwenyekiti, Rais Jakaya Kikwete Makamu Mwenyekiti Bara, Philip Mangula na wa Visiwani, Dk. Ali Mohamed Shein, huku Wilson Mukama aliyeingia madarakani kwa kuwapiga fitina viongozi waliomtangulia akienguliwa wadhifa huo alioutumikia kwa miezi 17 tu, na ukatibu Mkuu wa CCM ukatua kwa Abdulrahman Kinana.

Nyangwine: Sijaitelekeza Tarime

*Ajivunia maendeleo aliyowezesha

Mbunge wa Tarime mkoani Mara, Nyambari Nyangwine (CCM), ameibuka na kukanusha tuhuma za kutelekeza jimbo hilo kwa zaidi ya miezi sita mfululizo.

Usalama wa Taifa, TPA, Polisi, TRA wawajibishwe

Vyombo vya dola nchini, kwa mara nyingine vimeiaibisha nchi yetu kimataifa kwa kushindwa kudhibiti uvushaji wa shehena haramu ya meno ya tembo (ndovu) kwenda Dubai na hatimaye Hong Kong.

Na sisi tuchague makamishna wa polisi

ALHAMISI ya wiki iliyopita shule za msingi zilifungwa, watoto wakabaki majumbani na wazazi wao. Kwenye shule zao na katika vituo vingine mbalimbali, kulikuwa na kazi kubwa ya kisasa ya kuchagua makamishna wa polisi na uhalifu.