JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Maazimio Mkutano Mkuu: Kitanzi kinachoisubiri CCM

*Imeagiza bei za vifaa vya ujenzi zishushwe nchini

*Tofauti ya kipato yaelezwa ikiachwa hivi italeta vurugu

*Ada shule binafsi zidhibitiwe, utozaji dola ukomeshwe

*Yakiri ajira ni bomu, wizara lazima ziandae ajira mpya

*Ushuru na vijikodi vinavyoumiza wananchi vikomeshwe

Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Mkutano wake Mkuu wa Nane uliomalizika hivi karibuni mjini Dodoma, kilitoa maazimio ambayo kimeyaeleza kuwa ndiyo dira yake ya ushindi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2014 na Uchaguzi Mkuu mwaka 2015.

Wadau waaswa kuhusu takwimu sahihi

Sekta za umma, binafsi na wadau wa maendeleo kwa jumla, wameshauriwa kuzingatia matumizi bora kuwezesha upatikanaji wa takwimu sahihi na fursa kwa jinsia zote katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Bila flyover barabara hizi kazi bure

Ujenzi wa barabara unaendelea kwa kasi katika Jiji la Dar es Salaam. Lengo ni kuhakikisha kuwa foleni za magari zinapungua na hivyo kuondoa usumbufu na kuokoa mabilioni ya shilingi yanayoteketea kila siku. Tunaipongeza Serikali, na hasa Wizara ya Ujenzi kwa kazi hiyo nzuri ambayo inaonekana jijini humo na sehemu mbalimbali nchini.

Yah: Azimio la Arusha na ajira muhimu

Wanangu, leo ni Jumanne nyingine ambayo kwa uhakika imenifanya nikumbuke mambo mengi sana. Mojawapo ni yale maneno yaliyozungumzwa na Mwenyekiti wa TANU pale Mwanza Oktoba 17, 1967. Alizungumzia utekelezaji wa Azimio la Arusha.

…Mnyika: Chadema ngoma nzito

*Asema Chadema ina baraka za Mwalimu Nyerere

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetamba kwamba nguvu yake haitamalizwa na ziara za viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mikoani, katika kipindi hiki ambacho Watanzania wengi wanahitaji mabadiliko.

Vituo vya mafuta vinaiba kodi mchana kweupe

Mzee Ali Hassan Mwinyi alipata kusema maneno haya: “ Tanzania ni sawa na kichwa cha mwendawazimu.” Maneno haya aliyasema kwa maana kwamba kichwa cha mwendawazimu kila anayejifunza kunyoa hufanyia hapo mazoezi. Wiki iliyopita nilikuwa Nairobi , Kenya ambako nilikuwa na mafunzo ya wiki zaidi ya mbili. Nikiwa huko kwa mshangao nikakuta Tanzania inamwagiwa sifa.