JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Mwalimu Nyerere: Kujitolea kumefifia

“Siku hizi kuna watu wengi mno ambao huingia katika chama na kugombea nafasi za uongozi kwa matumaini ya kupata fedha na vyeo kwa faida zao wenyewe. Moyo wa kujitolea umefifia mno. Katika hali kama hiyo ni vigumu sana kuwapata viongozi wenye moyo wa kuwatumikia wenzao.”

Haya ni maneno ya Baba wa Taifa letu, Mwalimu Julius Nyerere, wakati akikemea tabia ya wanaotafuta uongozi kwa ajili ya maslahi yao binafsi. Alizaliwa Aprili 13, 1922 kijijini Butiama, Mara, alifariki Oktoba 14, 1999 jijini London, Uingereza.

Waliotoa rushwa waajiriwe polisi wanaugua ujinga

Tanzania inaelekea kuwa nchi ya watu walalamishi, wanaolia siku zote kulalamikia matatizo mbalimbali vikiwamo vitendo vya rushwa, ingawa wengi wao ni vinara wa kushawishi kutoa na kupokea rushwa. Cha kushangaza ni kwamba watoa rushwa ndio mara nyingi wamekuwa watu wa kwanza kulalamikia na kulaani uovu huo baada ya ‘kulizwa’ na wapokea rushwa katika mazingira mbalimbali.

Mwaka mmoja wa Jamhuri, tunawashukuru sana sana!

Desemba 6, 2012 Gazeti JAMHURI linatimiza umri wa mwaka mmoja. Mwaka mmoja si kipindi kirefu, lakini kwa uhai wa chombo cha habari, hasa katika mazingira ya nchi yetu, ni kipindi kirefu mno.

NSSF: Fao la kujitoa ni hatari

*Wananchi, Serikali wahadharishwa

*Machafuko ya kiuchumi yatatokea

*Yasema ikiamuriwa ina fedha za kulipa

Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) halijachoka kuwaasa Watanzania na Serikali juu ya athari za kutekelezwa kisheria kwa fao la kujitoa.

Dar es Salaam mpya

*NSSF kuanzisha miradi mikubwa jijini

*Mizigo bandarini kuondolewa kwa treni tano

*Mwisho wa malori kuingia jijini wawadia

*Nyumba zote Manzese, Vingungu kuvunjwa

Sura ya Jiji la Dar es Salaam itabadilishwa na kugeuka jiji la kisasa ndani ya miaka minne ijayo kutokana na mpango mzito ulioandaliwa na Mfuko wa Hifadhi za Jamii (NSSF).

Kwanini viwango vya wanasoka Tanzania vinashuka?

Tofauti na wanasoka, hasa washambuliaji mahiri wanaocheza Ligi Kuu za Ulaya kama Hispania, England na Ufaransa, straika wanaocheza Ligi Kuu ya Soka hapa nchini mara zote wameonesha kuwa wa msimu mmoja, siyo vinginevyo.