JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Madudu mengine TTCL

*Wasaini mkataba wa ulaji wa Sh milioni 740 kwa mwaka

*Walishirikiana na maofisa kuweka ‘walinzi hewa’ lindoni

Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), imeingia mkataba wenye utata na kampuni moja ya ulinzi wenye thamani ya Sh milioni 742 kwa mwaka. Utadumu hadi mwaka 2015.

Fisadi wa madini huyu hapa

*Amejenga ghala Chang’ombe, kazi inafanywa kwa siri

*Huyavusha hadi Nairobi kwa kuyaficha kwenye ngoma

Mfanyabiashara mwenye asili ya kiasia, anaendesha biashara ya siri ya kusafirisha mchanga wenye madini kutoka migodini na kufanya uchenjuwaji katika ghala lake lililopo Dar es Salaam.

Mwenyekiti Musukuma apuuzwe

Magazeti kadhaa yameripoti kwamba Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita, Joseph Musukuma, amewaambia wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji cha Nyawilimilwa kilichopo Kata ya Kagu, kwamba hatakuwa tayari kupeleka maendeleo katika kata hiyo kwa sababu inaongozwa na Diwani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Serikali isipuuze, udini upo, iudhibiti – 3

Wote tunakubali kuwa elimu ni ufunguo wa maisha. Kumnyima mtu au kundi moja ni sawa kumnyima mtu au kundi hilo maendeleo ya maisha yeke au yao katika uchumi madaraka, ajira na tija nyinginezo.

Mashindano ya Miss Tanzania yafutwe

Wakati huu wa harakati za kutoa maoni ya Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ni wakati mwafaka kutafakari kama mashindano ya ‘Miss Tanzania’ yanaikosea Tanzania.  Mwaka 1964 Serikali ilipiga marufuku mashindano hayo lakini yakaibuka kinyemela mwaka 1994 kwa mfano wa Azimio la Zanzibar, lililoibuka mwaka 1992 bila mwafaka wa kitaifa, na kuathiri Azimio la Arusha lililozaliwa mwaka 1967.

EfG inavyopinga ukatili kwa wanawake

Shirika lisilo la Serikali la Kuwezesha Wanawake Kibiashara (EfG) Tanzania, limekuwa mstari wa mbele kusaidia wafanyabiashara wasio katika sekta rasmi, ikiwa ni juhudi za kuinua nafasi zao katika nyanja mbalimbali ikiwemo ya kiuchumi.