JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Tumezubaa ardhi ya Tanzania inakwisha!

Mwaka 1958, Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, alizungumza maneno ya maana sana kuhusu ardhi.

 

Alisema, “Katika nchi kama yetu, ambayo Waafrika ni maskini na wageni ni matajiri, kuna uwezekano mkubwa kwamba Mwafrika akiruhusiwa kuiuza ardhi, katika miaka themanini au miaka mia ijayo, ardhi yote ya Tanganyika itamilikiwa na matajiri wageni, na wenyeji watakuwa watwana. Lakini hata kama wageni wasingekuwa matajiri, litaibuka tabaka la Watanganyika matajiri wajanja. Tukiruhusu ardhi iuzwe kama kanzu, katika muda mchache, kutakuwa na kundi dogo la Waafrika wakiwa na ardhi na walio wengi watakuwa watwana.”

Serikali isipuuze, udini upo, iudhibiti – 2

Inatoka toleo lililopita.

Jicho la kulia linaona dini ni mojawapo ya ngao zake katika kuwadhibiti na kuwahukumu raia wake wenye kutenda maovu au kwenda kinyume cha sheria za dola.

Baadhi ya maazimio ya CCM yametuhadaa

Ni jambo zuri kuona na kusikia Mkutano Mkuu wa Nane wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) umetoa maazimio ya kukiimarisha chama hicho tawala na kushughulikia changamoto mbalimbali nchini.

JKT ni mtima wa Taifa (4)

Leo nchi yetu ina vyama vingi, lakini cha kufurahisha kwangu mimi ni kuwa karibu viongozi wote wa vyama vya siasa wamehenya katika kambi za JKT kwa mujibu wa sheria. Ebu angalia hapa, Mwalimu Nyerere (Operesheni Mwenge Mafinga- siku moja), Rais Jakaya Kikwete (Operesheni Tumaini – Ruvu kwa Mujibu wa Sheria), Benjamin Mkapa (Operesheni Tekeleza Ruvu – Mature Age).

Mradi wa Nyumba za Bei Nafuu Mchikichini Wazinduliwa

Zitauzwa kwa wananchi wa kawaida, Waziri Tibaijuka aimwagia sifa NHC Watanzania wasio na viwanja sasa hawana sababu ya kuendelea kuhangaikia changamoto hiyo kwa vile Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limeanza kujenga nyumba za kuishi kwa ajili ya kuwauzia kwa bei nafuu.

Hongera Jamhuri, mmethubutu, mmeonesha njia

 

Naanza kwa kusema chereko chereko na hongera, pia kwa kutamka ‘Congratulations and Celebrations’ kwa gazeti Jamhuri kutimiza mwaka tangu kuingia sokoni mnamo Disemba 6, 2011 hadi leo. Vilevile natoa heko kwa waandishi wa habari kuliendesha gazeti hili hadi sasa, kwa umakini na utulivu, ndani ya soko la usambazaji wa habari kwa jamii.