JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Miaka 51 ya Uhuru, 50 ya Jamhuri: Tumekwama wapi?

Juzi Jumapili nchi yetu imetimiza miaka 51 ya Uhuru tangu tulipoupata Desemba 9, 1961 na mwaka mmoja baadaye ndhi yetu ikawa jamhuri. Kwa hiyo tumetimiza pia miaka 50 ya Jamhuri ingawa hili halitajwi sana.

Kituo cha Mabasi Ubungo: Mgodi wa mafisadi

*Hoja ya Mnyika yawekwa kapuni

Utangulizi

Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo (UBT) kilifunguliwa rasmi Desemba 6, 1999 pamoja na mambo mengine, uanzishwaji wa kituo hiki ulikuwa na madhumuni ya kutoa huduma kwa wasafiri pamoja na watumiaji wengine na pia kuongeza mapato ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.

RIPOTI MAALUMU

Chadema inakufa

*Mbowe, Dk. Slaa, Zitto, Shibuda hawapikiki pamoja

*Mabere Marando awatuhumu CCM, Usalama wa Taifa

*Heche, Waitara, Shonza kila mmoja lwake

*Kinana atema cheche, aeleza anachokifanya

 

Hali ya kisiasa ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ni mbaya na tayari kumeanza kuwapo hofu ya chama hicho kikuu cha upinzani hapa nchini, kufa.

Hofu hiyo inayokana, pamoja na mambo mengine, kuibuka kwa makundi yanayohasimiana, yanayoundwa na baadhi ya viongozi waandamizi wa chama hicho.

Kikwete alivyowalilia Sharo Milionea, Mlopelo, Maganga

Rais Jakaya Kikwete, ameelezea kustushwa na kusikitishwa na vifo vya wasanii maarufu nchini, Hussein Ramadhan Mkieti ‘Sharo Milionea’, Khalid Mohamed ‘Mlopelo’ na John Stephano Maganga.

Yanga inavyoipiku Simba

Hatua ya uongozi wa Yanga kuingia mkataba na kampuni ya kimataifa ya ujenzi inayojulikana kama Beijing Constructions ya China, imezidi kuwapiku mahasimu wake wakubwa wa soka nchini, Simba, kutokana na kuendelea kuwazidi kete ya mafanikio ndani na nje ya uwanja.

Fursa ya biashara ya mtandao duniani

Nianze kwa kuwasalimu wasomaji wetu ambao mmekuwa mkifuatilia safu hii kwa umakini mkubwa. Niwashukuru kipekee wote wanaonipigia simu, kuniandikia ujumbe mfupi (SMS) na baruapepe. Michango yenu wasomaji ina msaada mkubwa sana katika maeneo matatu.

Mosi, inanipa taarifa kwamba ninachokiandika kinasomwa.