JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Wabunge waichachafya Katiba

*Jaji Warioba, Mbunge walumbana ukumbini

Wabunge kadhaa wameikosoa Katiba ya sasa ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na wametoa mapendekezo mazito wakipendekeza yaingizwe kwenye Katiba mpya.

Kenya, Uganda, Rwanda wanatuacha solemba

Kwa zaidi ya wiki sasa nipo hapa Nairobi, Kenya, nikihudhuria mafunzo ya uandishi wa habari za masuala ya kifedha, hasa bajeti ya Serikali. Mafunzo haya ni ya muda wa wiki mbili. Katika mafunzo haya tunapewa mifano kutoka sehemu mbalimbali na wakubwa kutoka Serikali ya Kenya wanawasilisha mada.

Dk. Nagu alichomfanyia Sumaye

Barua hii imeandikwa na watu waliojitambulisha kuwa ni wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambao ni Wajumbe wa Mkutano Mkuu Wilaya ya Hanang’. Iliandikwa Oktoba 19, mwaka huu na kupelekwa kwa Katibu Mkuu wa CCM-Taifa. Kimsingi inapinga ushindi wa nafasi ya NEC wa Dk. Mary Nagu dhidi ya Waziri Mkuu mstaafu Frederick Sumaye.

YAH: KUPINGA MATOKEO YA UCHAGUZI NAFASI YA MJUMBE WA HALMASHAURI KUU TAIFA (NEC) WILAYA YA HANANG’

Mheshimiwa Katibu Mkuu, kichwa cha habari hapo juu chahusika. Sisi wenye majina na saini zetu hapo chini kwenye kiambatanisho cha barua hii ni viongozi na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM (W) ya Hanang’.

 

Mtikisiko mkubwa CCM

*Msekwa, Karume kutemwa rasmi, vigogo wengi kuangukia pua

*Wasira, Lukuvi, Membe, Makamba, Mukama wapambana

*Balozi Seif, Shamsi, Khatib, Mbarawa, Samia, Mwinyi vita kali

Wiki hii Chama Cha Mapinduzi (CCM) kitakuwa katika hatua za mwisho za kukamilisha safu zake za uongozi, huku mtikisiko mkubwa ukitarajiwa kutokea kwa vigogo wengi kubwagwa kwenye nafasi ya ujumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) – viti 10 Bara na viti 10 Zanzibar.

Maximo alishindwa, nani atamvumilia Boban?

Moja ya uamuzi mgumu uliofanywa na uongozi wa Klabu ya Simba ya Dar es Salaam, ni kumsimamisha mchezaji wake, Haruna Moshi ‘Boban’, kwa kosa la utovu wa nidhamu.

Watanzania tunapaswa kuongeza ‘akili ya fedha’

Mapema Julai mwaka huu, nilikutana na mzee mstaafu kutoka moja ya wilaya za mkoani Iringa. Mzee huyu ambaye ndiyo kwanza amestaafu  ualimu, nilimfahamu kwa njia ya simu kupitia kwa rafiki yangu. Haja ya mzee huyu ilikuwa tukutane nimsaidie kutafuta gari aina ya Hiace anunue.