JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Mwenyekiti Musukuma apuuzwe

Magazeti kadhaa yameripoti kwamba Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita, Joseph Musukuma, amewaambia wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji cha Nyawilimilwa kilichopo Kata ya Kagu, kwamba hatakuwa tayari kupeleka maendeleo katika kata hiyo kwa sababu inaongozwa na Diwani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Serikali isipuuze, udini upo, iudhibiti – 3

Wote tunakubali kuwa elimu ni ufunguo wa maisha. Kumnyima mtu au kundi moja ni sawa kumnyima mtu au kundi hilo maendeleo ya maisha yeke au yao katika uchumi madaraka, ajira na tija nyinginezo.

Mashindano ya Miss Tanzania yafutwe

Wakati huu wa harakati za kutoa maoni ya Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ni wakati mwafaka kutafakari kama mashindano ya ‘Miss Tanzania’ yanaikosea Tanzania.  Mwaka 1964 Serikali ilipiga marufuku mashindano hayo lakini yakaibuka kinyemela mwaka 1994 kwa mfano wa Azimio la Zanzibar, lililoibuka mwaka 1992 bila mwafaka wa kitaifa, na kuathiri Azimio la Arusha lililozaliwa mwaka 1967.

EfG inavyopinga ukatili kwa wanawake

Shirika lisilo la Serikali la Kuwezesha Wanawake Kibiashara (EfG) Tanzania, limekuwa mstari wa mbele kusaidia wafanyabiashara wasio katika sekta rasmi, ikiwa ni juhudi za kuinua nafasi zao katika nyanja mbalimbali ikiwemo ya kiuchumi.

Je, ushirikina unafanikisha biashara?

Mapema mwaka huu nilikuwa miongoni mwa maelfu ya wakazi wa mji wa Iringa, waliokwenda kushuhudia sakata la misukule katika Frelimo, iliyodaiwa kuwa kwenye nyumba ya mama mmoja mfanyabiashara maarufu mjini hapa. Licha ya kufika mapema sana eneo hilo lakini sikubahatika kuona misukule!

NHC yazidi kujiimarisha

*Kasi ujenzi nyumba za makazi, vitegauchumi yaongezeka

*Nyumba 1,000 kwa wenye kipato kidogo kujengwa mikoa 14

Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) linaendelea kutimiza dhima ya kuanzishwa kwake kwa kuhakikisha linatekeleza miradi mbalimbali ya ujenzi wa nyumba za makazi na vitega uchumi.

Kwa sasa NHC imekamilisha baadhi ya miradi, mingine inaendelea na pia imejiwekea mpango mkakati wa kuendelea na ujenzi wa nyumba kwa mahitaji mbalimbali nchini.