JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Ufisadi washamiri TTCL

*Mabilioni ya makusanyo yayeyuka

Wakati Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, January Makamba, alitarajiwa kukutana na wafanyakazi wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) jana, viongozi wakuu wake wanatuhumiwa kufanya ufisadi unaoiangamiza kampuni hiyo ya umma.

IGP Mwema heshima uliyoijenga inapotea

Miezi ya Desemba 2012 na Januari, 2013 imenitia hofu. Imenitia hofu baada ya kuwapo matukio mengi ya wizi, ujambazi na ukatiri dhidi ya binadamu. Wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha wamelazimia kuandamana baada ya majambazi kuwa wanawavamia kwenye mabweni yao na kuwapora kompyuta za mkononi, fedha na vitu vya thamani. Imeelezwa kuwa hadi wanafikia uamuzi huo tayari walikwishaporwa laptop zipatazo 300.

TCRA kuvifungia vituo vya runinga

Siku za vituo vya runinga ambavyo havijajiunga na mfumo mpya wa dijitali nchini zinahesabika.

Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania (TCRA), imetangaza kuvinyang’anya leseni vituo hivyo ikiwa vitaendelea kukaidi agizo hilo la Serikali.

JAMHURI yafanikisha kukamatwa ‘majangili’

Wizara ya Maliasili na Utalii imewatia mbaroni watuhumiwa wa ujangili katika Kijiji cha Mkata, Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro.

Kashfa mpya Red Cross

*Dk. Nangale ‘achukua’ mitambo ya redio

Redio ya Sibuka imeingia katika kashfa nzito baada ya kubainika kuwa mitambo inayotumia redio hiyo kurusha mawimbi ya sauti ni mali Chama cha Msalaba Mwekundu (TCRS).

Ukabila watikisa Uhamiaji

*Wafanyakazi wamwandikia Waziri waraka

*Waorodhesha majina 70 ya wanaowatuhumu

*Mkutano wa wafanyakazi waitishwa, waonywa

Wafanyakazi wa Idara ya Uhamiaji walioficha majina, wamemwandikia Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. John Nchimbi, waraka wakilalamikia vitendo vya ukabila ndani ya Idara hiyo. Katika waraka huo, wamedai kwamba karibu nafasi zote nono zimeshikwa na makabila mawili pekee yanayotoka Mkoa wa Kilimanjaro.