JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

FASIHI FASAHA

Tunakubali rushwa ni adui wa haki?

“Rushwa ni adui wa haki; sitapokea wala kutoa rushwa.”

Nimeanza na kauli hiyo kwa dhamira ya kukumbuka na kuuliza, “Wazalendo wa Tanzania wameikubali, wameizingatia na wanaitekeleza?”

FIKRA YA HEKIMA

Wanafunzi IFM nao wachunguzwe

Kero za uvamizi, uporaji mali, ubakaji na ulawiti dhidi ya wanafunzi wa Taasisi ya Usimamizi wa Fedha (IFM), zitapatiwa ufumbuzi wa kudumu ikiwa uchunguzi unaofanywa na Jeshi la Polisi utawalenga pia wanafunzi hao.

CHADEMA: Tunataka Serikali tatu – 2

Wiki iliyopita tulichapisha sehemu ya kwanza ya maoni ya Chadema kwa Tume ya Marekebisho ya Katiba. Sehemu ya kwanza iliahidhi kuwa sehemu ya pili ya mapendekezo haya itaanzia kwenye mtazamo wa Chadema juu ya uwapo wa Serikali ya Tanganyika. Endelea…

Dk. Wanyanja: Rais apunguziwe nguvu

*Apendekeza rais anapotuhumiwa apelekwe mahakamani

*Asitumie walinzi, magari ya Serikali wakati wa kampeni

*Kuwepo serikali 3 ikiwamo ya Tanganyika , Bunge, SenetiAliyekuwa Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk. James Wanyancha (pichani), ametoa mapendekezo yake ya Katiba na kutaka rais aondolewe kinga kushitakiwa mahakamani.

Muungano ndiyo mboni ya Tanzania (7)

Watu mnaweza kubishana kwa hoja, lakini si kwa kukamiana nani ni nani Visiwani Zanzibar. Kila mtu anataka, na ni haki yake kila mwananchi kutambuliwa kama yupo. Kutambuliwa huko kunafikiwaje? Vyama vyote vya upinzani vina lengo kuu moja tu- kuingia serikalini na kuboresha maisha ya wananchi kiuchumi, kielimu, kiafya na kiutawala bora. Njia zipi zitumike kuyafikia malengo hayo? Ndiyo ngoma inayochezwa kwenye uchaguzi huru.

Hongera DC, Mahakama lakini sheria mbovu

WIKI iliyopita vyombo vya habari nchini vilichapisha habari kuwa Mahakama ya Wilaya Bunda imemtia hatiani na kuamuru afungwe jela miaka mitatu mfanyabiashara mwenye asili ya Kichina, Mark Wang Wei aliyejitoa wazi kumhonga Sh 500,000 Mkuu wa Wilaya hiyo, Joshua Mirumbe.