JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Balozi Finland: Misitu inaweza kuiinua Tanzania

Misitu ina nafasi kubwa ya kukuza uchumi wa Watanzania ikiwa itatumiwa vizuri, amesema Balozi wa Finland hapa nchini, Sinikka Antila.

JAMHURI yaisafisha TTCL

Bodi ya Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), imemng’oa katika madaraka Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo, Said Amir, na kuwasimamisha kazi maofisa wengine watatu waandamizi ili kupisha uchunguzi kuhusu tuhuma za ufisadi zinazowakabili.

Mangula kazima moto kwa petroli Bukoba

Kwa karibu miezi sita sasa, siasa za Jimbo la Bukoba mjini zimegeuzwa siasa za chuki, kutishana, fitina, kuchambana, kulaumiana, kuonesha umwambwa, uwezo wa kifedha, dharau, ubaguzi  na ujenzi wa matabaka yanayosigana katika jimbo hili.

Milioni 826/- zayeuka Shirika la Bima Taifa

Uongozi wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) unakabiliwa na tuhuma za kukilipa kiwanda cha pamba kilichofilisika, Sh milioni 826 bila maelezo ya kuridhisha.

Kagasheki atiwa majaribuni

Kundi la wafanyabiashara kadhaa wa tasnia ya uwindaji wa kitalii, limekutana nchini Marekani na kuendesha mchango wa mabilioni ya shilingi kufanikisha ugawaji upya wa vitalu vya uwindaji.

Vinara mgogoro wa gesi watajwa

Matajiri wakubwa nchini wanaojihusisha na biashara ya mafuta ya petroli, mafuta mazito ya viwandani na kampuni kubwa za kimataifa, ni miongoni mwa wanaochochea mgogoro wa kupinga ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara kwenda Dar es Salaam , JAMHURI imethibitishiwa.