JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Wao na mashangingi, masikini na sakafu

Rais Paul Kagame wa Rwanda alipotwaa madaraka, miongoni mwa “uamuzi mgumu” wa awali aliouchukua ni kuhakikisha anapunguza matumizi yanayosababishwa na magari ya umma. Akayakusanya kwa wingi. Akayaweka uwanjani. Akapewa orodha ya maofisa na watumishi wanaostahili kukopeshwa magari. Akawaagiza waende uwanjani- kila mmoja achague analotaka. Akahakikisha aliyechagua gari anakopeshwa-linakuwa mali yake. Huduma za mafuta na matengenezo zikaandaliwa utaratibu kwa kila gari na kwa muda maalumu.

fasihi fasaha

Tunakubali rushwa ni adui wa haki? (4)

Ni miaka 17 sasa tangu Tume ya Kero ya Rushwa ilipotufahamisha mianya na sababu za kuwepo rushwa, wala rushwa na njia za kuitokomeza. Lakini kilio kikubwa cha madhara ya rushwa bado kinasikika kutoka kwa wananchi.

FIKRA YA HEKIMA

Tunahitaji rais dikteta mwenye uzalendo

Jumamosi iliyopita wakati jua likielekea kuchwea, nilihisi faraja kuandaa makala hii kutoa changamoto kwamba nchi yetu sasa inahitaji kuwa na rais dikteta lakini aliye mzalendo. Dikteta ni mtu anayetawala nchi kwa amri zake bila kushauriwa, au anayetaka analosema litekelezwe bila kupingwa, na mzalendo ni mtu anayependa nchi yake kiasi cha kuwa tayari kuifia.

Ni ujinga CHADEMA kupinga uzazi wa mpango – (2)

Amani Golugwa amendelea kudai kuwa wasomi wengi wameshangazwa na kauli ya Rais Kikwete ya kuwataka Watanzania wafuate uzazi wa mpango. Huo ni uzushi ambao CHADEMA ni kawaida yao.

Sagara: Katiba izuie wastaafu kurejeshwa kazini

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime mkoani Mara, Amos Sagara (pichani chini), amependekeza Katiba mpya izuie wastaafu kurejeshwa katika utumishi wa umma.

Utawala Bora hutokana na maadili mema (2)

 

Mara baada ya Uhuru baadhi ya wageni kwa dharau za makusudi kabisa walijaribu kuchezea uwezo wa Serikali ya Taifa letu huru. Nitoe mifano ya dharau za namna hiyo.