JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Serikali imdhibiti mwekezaji huyu

Moja ya habari zilizobeba uzito wa juu katika gazeti hili ni ile inayomhusu raia wa Uswisi, Dk. George Hess, anayetuhumiwa kumiliki na kuuza ufukwe wa Amboni uliopo Wilaya ya Muheza, mkoani Tanga kinyume cha sheria.

Kasi yetu ya kuchimba dhahabu inatisha, idhibitiwe – 2

Wiki iliyopita makala haya yalihoji kwa nini hakuna anayeingia mgodini kupinga uchimbaji wa kasi kubwa bila udhibiti. Leo tunakuletea sehemu ya pili ya makala haya. Endelea…

Rais Karume, Maalim Seif ni Uamsho?

Kwa muda sasa nchi yetu imetikiswa. Imetikiswa si na kingine, bali ishara na viashiria vya udini. Tumepata misukosuko huko Buseresere kwa Wakristo kuamua kuchinja. Tumepata misukosuko huko Zanzibar kwa Padre Evarist Mushi kupigwa risasi na Kanisa kuchomwa moto.

Medeye afichua siri migogoro ya ardhi Arumeru

Mbunge wa Arumeru Magharibi, Gooluck ole Medeye (CCM), ameibuka na kuanika siri ya migogoro ya ardhi katika Wilaya ya Arumeru, mkoani Arusha.

Nchi inavyoliwa

[caption id="attachment_695" align="alignleft" width="266"]Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Galawa[/caption]Raia wa Uswisi, Dk. George Hess, anatuhumiwa kujimilikisha na kuuza ardhi ya ufukwe wa Amboni uliopo Wilaya ya Muheza, mkoani Tanga, kinyume cha sheria. Dk. Hess, anayeishi nchini Kenya, kupitia tovuti yake ya ambonibeach.com, amejitangazia ‘Jamhuri’ katika eneo hilo, kuwa ndiye mmiliki pekee Tanzania mwenye ufukwe, jambo ambalo ni kinyume cha Sheria ya Ardhi namba 4 ya mwaka 1999.

Sheria ya Mipango Miji namba 7 ya mwaka 2008 na Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004, inakataza mtu yeyote kumiliki ufukwe wa bahari bali fukwe zinapaswa kumilikiwa na umma. Lengo la kutungwa kwa sheria hiyo ni kuhakikisha fukwe hazihatarishi amani, ulinzi na usalama wa raia.

Lissu, Mrema, Mbowe wamsulubu Kikwete

[caption id="attachment_693" align="alignleft"]Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu[/caption]*Wasema nchi imemshinda, watapika nyongo
*Wasema Serikali inaandaa taifa la wajinga

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema, Freeman Mbowe, Mbunge wa  Singida Mashariki, Tundu Lissu na Mwenyekiti wa Tanzania Labor Party (TLP), Agustino Mrema, wametoa tuhuma nzito kuwa nchi imemshinda Rais Jakaya Kikwete.