JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Arusha yazizima

Vifo visivyotarajiwa vya wafanyabiashara maarufu wawili – Henry Nyiti na Nyaga Mawalla – vimeibua hisia tofauti miongoni mwa wakazi wa Arusha na mikoa ya kaskazini kwa jumla. Nyiti alikuwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni iliyojihusisha na uchimbaji na uuzaji vifaa vya madini ya Interstate Mining and Mineral,s iliyokuwa na makazi yake mkoani Arusha.

Lwakatare alivyorekodiwa

Taratibu mambo yameanza kuwekwa hadharani, na sasa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinasema Mkurugenzi wao wa Idara ya Ulinzi, Wilfred Lwakatare, alirekodiwa na msaidizi wake, Joseph Ludovick. Hata hivyo, wakati Chadema wakiibua hayo, wanasema wanao ushahidi mzito unaonesha kuwa Ludovick alirubuniwa na Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Mwigulu Nchemba, kufanya uharamia huo.

NUKUU ZA WIKI

Nyerere: Elimu inayotolewa ituwezeshe kujiamini

“Elimu inayotolewa lazima ijenge akili ya kuuliza, uwezo wa kujifunza na uwezo wa kujiamini kama raia huru na sawa katika jamii.”

Maneno haya ni ya Mwasisi na Baba wa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Udini sasa nongwa (2)

Ningependa nioneshe pia kuwa wapo wasomi wasiojiamini kabisa ingawa wana shahada za vyuo viikuu. Kama si upotoshaji wa kukusudia, basi hawana elimu (not liberated mentally), ni wajinga ingawa wamesoma (have been to school but not educated).

Kamati ya wadau wa habari ituondolee hofu

Wiki iliyopita, wadau wa habari kupitia Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT), waliunda kamati ya watu 16 kwa ajili ya kukutana na wakuu wa vyombo vya usalama nchini.

Pole sana kaka Absalom Kibanda

Ninahuzunika juu yako kaka yangu Absalom Kibanda. Moyo wangu umejaa uchungu. Kibanda wamekutenda vibaya, wamekuteka, wamekushambulia na kukujeruhi vibaya! Wamekusababishia kilema.