JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Ni Bajeti ya Karne ya 22

*Asilimia 90 ya Bajeti ya Wizara zapelekwa kwenye maendeleo

*Wamarekani wamwaga mabilioni mengine kwenye MCC

*Mtwara, Lindi wapendelewa, kuunganisha umeme Sh 99,000

*Wizara yasisitiza ujenzi bomba kutoka Mtwara upo palepale

 

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, amesoma Bajeti ya wizara hiyo ya mwaka wa fedha wa 2013/2014 na kusema asilimia 90 ya fedha zinazoombwa ni kwa ajili ya maendeleo; na hivyo kuifanya kuwa ni maalumu kwa ajili ya kuiingiza Tanzania katika karne ya 22.

Vurugu zaua JWTZ 4 Mtwara

*Upuuzi, uhuni vyafanywa katika mitaa

*Kisingizio cha gesi chatumika kufanya uasi

*Nyumba ya Waziri, CCM, umma zateketezwa

 

Vifo vya watu kadhaa vimeripotiwa kutokea mkoani Mtwara vikisababishwa na vurugu za wananchi walioamua kuchoma mali za watu binafsi, umma na taasisi mbalimbali.

Dhahabu ya mabilioni yakamatwa ikitoroshwa

Serikali imekamata madini yenye thamani ya Sh bilioni 13.12 yaliyokuwa yakisafirishwa nje ya nchi kinyume cha sheria kwa kipindi cha kuanzia Oktoba, 2012 hadi Aprili, mwaka huu.

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, alitoa taarifa hiyo kwenye hotuba yake ya bajeti ya mwaka wa fedha wa 2013/2014 bungeni, jana.

Tanzania haiwaamini makocha wa kigeni

Hivi sasa watu duniani wanaonekana kupenda mchezo wa soka zaidi kuliko michezo mingine, na mezzo huo umekuwa ukiongeza ajira kwa vijana kila kukicha.

Vurugu za Mtwara ni uhuni na upuuzi

Kwa mara nyingine, wahuni kadhaa katika Mji wa Mtwara jana waliendesha vitendo vya uvunjifu wa amani. Watu kadhaa wameripotiwa kuuawa, kujeruhiwa na mali za mamilioni ya shilingi zimeteketezwa.

RIPOTI MAALUMU

Mtandao wa mauaji ya Barlow watajwa

*Jambazi atinga bungeni, afungua makabrasha mpango ulivyosukwa

 

*Awataja polisi, usalama walivyohusika, JWTZ yamwokoa asiuawe

 

*Pinda aelekeza alindwe, Nchimbi akiri kupata taarifa za kutisha

Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Liberatus Barlow, aliuawa na genge la uhalifu ndani ya Jeshi la Polisi, siri zilizovuja zimeifikia JAMHURI.