JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Ndoto ya pensheni kwa wazee wote kutimia (1)

 

Siku za karibuni tumesikia misamiati mbalimbali juu ya kuwasaidia wazee wote wa Tanzania. Upo msamiati wa wazee kupatiwa PENSHENI huko tuelekeako. Wengine wanasema wazee watapata Cash Grant. Msamiati mwingine unasema wazee wanaandaliwa mpango unaojulikana kama Universal Pension Scheme. Kitaifa ipo mifumo kadhaa ya kuwasaidia watu inayoitwa Mifuko ya HifadhiI ya Jamii kama vile NSSF, PPF, NHIF na LAPF.

Mauaji ya Barlow wingu zito latanda

*Polisi wasema kijana aliyetaja mtandao ni mgonjwa wa akili

*Yeye asisitiza kuwa kichaa, analazimishwa dawa Muhimbili

*Ndugu waeleza historia, daktari anayemtibu aingia mitini

Jeshi la Polisi nchini limempeleka na kumlaza katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, kijana Mohamed Malele, mshirika wa mtandao uliohusika kumuua Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Liberatus Barlow, wakidai ni mgonjwa wa akili.

RPC ‘atumika’ kuchangisha rushwa

* Watendaji wadaiwa kutumia jina lake kula rushwa kwa walima bangi

* RPC Tarime/Rorya awaruka, DC asema dawa yao inachemka

Maofisa watendaji wa Kijiji cha Kwisarara na Kata ya Bumera wanatuhumiwa kutumia jina la Kamanda wa Polisi wa Mkoa (RPC) wa Kipolisi Tarime/Rorya kuchukua rushwa ya fedha kutoka kwa wakulima wa zao haramu la bangi.

Rage ni tatizo Simba-Kalimauganga

Mwenyekiti wa Friends of Simba, Mkoa wa Tabora, Sadiki Kalimauganga, amesema kuwa kufanya vibaya kwa Wekundu wa Msimbazi Simba Sports Club ya Dar es Salaam, katika Ligi Kuu ya Vodacom iliyomalizika hivi karibuni, kunatokana na uongozi mbovu wa Ismael Aden Rage.

Diwani awaangukia wezi wa sola

Diwani wa kata ya Kisaka wilayani Serengeti, Chacha Togoche, ‘amewangukia’ wezi akiwaomba kutorudia kuiba sola katika zahanati ya kijiji cha Nyiboko.

Wabunge maslahi watalipeleka taifa msituni

Wiki iliyopita nilijizuia kuandika juu ya Bunge na wabunge wetu. Nilijizuia baada ya kusikiliza mjadala uliokuwa unaendelea bungeni, nikawasikiliza wabunge maslahi wanaochangia kwa nguvu hadi wanatokwa na povu midomoni, bila kulieleza Bunge sawa bin sawia kuwa maumivu waliyopata kwa wanahabari yanatokana na maovu yao.