JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

RASIMU YA KATIBA YA TANZANIA 2013

Hofu yatanda Z’bar

*Walio Tanganyika kugeuka wawekezaji

*Wasiwasi watanda, wanunua ardhi Bara

*Wahoji Tume ya Warioba kufuta Takukuru

Mapendekezo ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya ya kuondoa suala la ardhi katika mambo ya Muungano, yamezaa hofu kwa Wazanzibari wanaoishi Tanzania Bara na ndugu zao walioko Zanzibar.

….Makundi ya urais yayeyuka

Rasimu ya Katiba Mpya imeyanyong’onyeza makundi ya wanaowania urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa muda mrefu kumekuwapo mjadala mkali wa nani anayestahili kuwania kiti hicho, lakini mbio hizo zimepunguzwa kasi na umaarufu wake, baada ya rasimu kupendekeza kuwapo kwa muundo wa Serikali Tatu – Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, na Tanzania Bara (Tanganyika).

Vidonda vya tumbo na hatari zake (1)

ijmc

Miili yetu hutegemea vyanzo viwili vya nguvu ambavyo ni oksijeni na vyakula. Oksijeni huingizwa ndani ya miili yetu kupitia pumzi na kuingia moja kwa moja katika utendaji, wakati chakula hutakiwa kupitia mchakato mrefu kuweza kutumiwa na mwili.

Kijana Malele adhalilishwa kutangazwa kichaa

Kijana aliyejitangaza kung’atuka ushirika wa mtandao unaodaiwa kuhusika kumuua Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Liberatus Barlow, anaweza kulalamikia kitendo cha kudhalilishwa kwa kumtangaza kuwa ni mgonjwa wa akili.

Mil 200/- zatafunwa ‘mradi hewa’ Geita

Shilingi milioni 200 zilizotengwa kwa ajili ya ujenzi wa skimu ya umwagiliaji katika vijiji vya Nyamboge kilichopo Kata ya Katoma; na Nzera katika Kata ya Nzera, Wilaya ya Geita mkoani, ‘zimeyeyuka’.

Mengi aanzisha shindano kukabili umaskini Tanzania

. Watu wanatuma mawazo bunifu kupitia Tweeter

. Washindi wazawadiwa Sh mil 1.8 kila mwezi

Katika juhudi za kutafuta ufumbuzi wa umaskini Tanzania, Mwenyekiti wa kampuni za IPP, Dk. Reginald Mengi, ameanzisha shindano la mawazo mapya yanayotaja mbinu bora za kutokomeza tatizo hilo.